• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

ONGEZENI NGUVU YA UZALISHAJI KUFIKIA SERA YA UCHUMI WA VIWANDA -DC KILOSA

Posted on: September 13th, 2018

Sera ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Rais John Pombe Magufuli ni kujenga uchumi wa viwanda na kwamba ili kuhakikisha sera hii ya kuwa na uchumi wa viwanda inafanya kazi wadau mbalimbali wa kilimo wilayani Kilosa na hasa idara ya Kilimo Ushirika na Umwagiliaji wametakiwa kuongeza nguvu ya uzalishaji kwani kilimo kwa asilimia kubwa huchangia pato kubwa hapa nchini.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi wakati wa kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mpango Mkakati kwa mwaka 2017/2018 ambapo mpango huo umepangwa kukamilika ifikapo 2020 ambapo amesema kuwa Halmshauri ina wajibu mkubwa katika kutimiza mpango huo kwa kuongeza juhudi  za uzalishaji utakaosaidia kupata mapato ya ndani yatakayosaidia kuhudumia wananchi.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale ameitaka bodi ya pamba kuwa na mawakala wengi wanaosambaza viuatilifu vya pamba ili Halmashauri iweze kuwa na wigo mkubwa wa kuchagua kampuni wanayoitaka kuliko hali ilivyo sasa ya kuwa na kampuni moja tu ambayo imepekekea kujitokeza kwa changamoto ya ucheleweshaji wa pembejeo za kilimo na nyingine kushindwa kufanya kazi ipasavyo,ambapo pia ametaka utaratibu wa kupima sucrose kwenye miwa ufanyike kwa uwazi kati ya kiwanda na wakulima sambamba na ushirikishwaji wa wakulima ili kufanikisha utendaji wa haki.

Aidha Mkuu wa Idara ya Kilimo Wilaya Tatu Kachenje amesema kuwa mpango wa kuboresha kilimo una lengo la kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara kwa eneo kupitia mnyororo wa thamani ifikapo 2020 ambapo katika utekelezaji wake kwa mwaka 2017/2018 eneo lililolimwa mwaka huu limeongezeka na kufikia hekta 252,799.8 ya eneo la hekta 417,210 linalofaa kwa kilimo ambapo nguvu kubwa kwa msimu uliopita ilitumika katika kuhamasisha na kuelimisha jamii katika mazao mbalimbali yakiwemo ya  chakula, mazao ya kimkakati kama vile pamba, korosho na miwa.

Pamoja na utekelezaji huo Kachenje amesema walikutana na changamoto mbalimbali ikiwemo uhaba na kuchelewa kwa mvua, kutokea kwa mafuriko, uwepo wa visumbufu vya mazao,migogoro ya wakulima na wafugaji,uhaba wa vitendea kazi, baadhi ya viuatilifu vya pamba kutofanya kazi vizuri, ubovu wa miundombinu na mbegu bora ya miwa kutopatikana kwa mtiririko mzuri.

 Kachenje amesema mpango huo umelenga ifikapo Juni 2018 uwe umeongeza uzalishaji wa mazao ya chakula,uzalishaji mazao jamii ya mizizi, kuimarisha mbinu za uhifadhi wa mazao baada ya mavuno, kuongeza uzalishaji mazao ya biashara, kuboresha kilimo cha mboga mboga na matunda, kuboresha mfumo wa masoko kwa mazao ya kilimo, kuongeza uzalishaji wa mbegu daraja la kuazimiwa ubora kupitia vikundi, kuboresha eneo la umwagiliaji, kuimarisha vikundi 10 vya umwagiliaji katika uendeshaji na utunzaji wa miundo mbinu ya kilimo, kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi, kuimarisha mbinu bora za kuboresha afya ya udongo  na kuanzisha majukwaa ya mazao ya biasha

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa