• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

RC MALIMA AITAKA HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOSA KUWEKEZA KWENYE KILIMO CHA MAZAO YA KIMKAKATI

Posted on: June 25th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima ameitaka Halmashauri ya wilaya ya Kilosa kuyapa kipaumbele mazao ya kimkakati kama vile kokoa ili kuinua uchumi wa wananchi na pato la Halmashauri kwa ujumla.

Mhe. Malima ametoa rai hiyo wakati wa mkutano maalumu  wa baraza la madiwani wa kujadili taarifa ya utekelezaji wa mapendekezo ya mdhibiti na mkaguzi wa fedha za serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2022/2023 uliofanyika June, 25, 2024 katika ukumbi wa Chuo cha Maendeleo  (FDC)  Ilonga.

Amesema kuwa kuna haja ya kuwafundisha wananchi namna bora ya kulima mazao hayo ili yawe na tija kwao huku akitaka mifumo maalumu ya kuuza na kununua kama vile Stakabadhi Ghalani ifuatwe ili wakulima wanufaike.

Katika hatua nyingine, RC Malima amezipongeza Halmashauri za mkoa wa Morogoro kwa kuwa na hoja chache zinazoibuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi wa Serikali (CAG) na kuwataka watendaji pamoja na Waheshimiwa Madiwani kukaa mara kwa mara kuzipitia hoja zilizoibuliwa na kuzimaliza.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mussa Ali Musa amewataka wananchi wa Kilosa kuchangamkia fursa za Uwekezaji katika mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) ambayo itaanza kutumika hivi karibuni huku akiwataka viongozi wa wilaya kutengeneza mazingira mazuri ya uwekezaji.

Amezitaja fursa kama vile vituo vya magari, migahawa, hoteli na kadharika kuwa zinaweza kuwa chachu ya maendeleo kutokana na kuwepo kwa reli hiyo.

Naye mkuu wa wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka ameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia wilaya ya Kilosa miradi mingi ya maendeleo na kuahidi kuendelea kuisimamia vizuri ili iwanufaishe wananchi wa Kilosa.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa mapendekezo ya CAG kwa mwaka wa fedha wa 2022/2023, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kilosa Michael J. Gwimile amesema kuwa Halmashauri ilifanikiwa kupata hati safi ikiwa ni mwaka wa tisa mfululizo.

Aidha amesema kuwa mpaka mpaka sasa hoja takribani 5 ndizo zilizosalia kati ya hoja 12 zilizoibuliwa na CAG kwa mwaka wa fedha 2022/2023 na kuahidi kuwa hizo zilizobaki zitatatuliwa.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa