• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

RC MALIMA ATEMBELEA MAENEO YALIYOATHIRIKA NA MAFURIKO KILOSA NA KUAHIDI MISAADA YA KIBINADAMU KWA WAHANGA

Posted on: December 6th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adamu Malima amefanya ziara katika kata za Rudewa na Mvumi Wilayani Kilosa ili kujionea madhara yaliyosabaishwa na mafuriko yaliyozikumba kata hizo usiku wa kuamkia Disemba 05,2023 na kuahidi misaada ya kibinadamu ikiwemo chakula na huduma za afya kwa wahanga wa mafuriko hayo.

Mhe. Malima amefanya ziara hiyo Disemba 06,2023 na kueleza kuwa serikali ya mkoa itachangia mahitaji kama vile chakula, malazi, mavazi  kama sehemu ya kuwasaidia waathirika wa mafuriko hayo.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa ameziagiza mamlaka za TANESCO, TARURA, RUWASA na Mamlaka za barabara kurejesha huduma za maji, umeme na miundombinu ya barabara ili kuwaezesha wakazi wa maeneo hayo kurejea katika maisha yao ya kawaida.

Hata hivyo, amesema kuwa katika tathimini ya awali iliyofanywa na kamati ya maafa ya wilaya imebainisha kuwa zaidi ya nyumba 100 zimeathirika na mafuriko hayo huku watu watatu wakifariki kutokana na mafuriko hayo.

Mkuu huyo wa Mkoa pia ametahadharisha baadhi ya watu wanaowaibia wahanga vitu na mali zao kuacha mara moja tabia hizo na kuziagiza mamlaka za ulinzi na usalama kulifanyia kazi suala hilo.

Katika kulikabili hilo, Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka ambaye aliambatana na Mkuu wa Mkoa katika ziara hiyo amebainisha kuwa kwa kushirikiana na mamlaka za polisi watahakikisha wanawadhibiti watu wenye nia ya kuwaibia waathirika wa mafuriko hayo

Kwa upande wake Meneja wa mamlaka ya maji safi na salama Mkoa wa Morogoro (RUWASA) Mhandisi Sospita Mtondwa amesema kuwa wameshachukua hatu za awali za kuhakikisha maji yanayopatika katika maeneo yalioathirika na mafuriko ni safi na salama kwa kuweka dawa kwenye maji yaliyotuama ili yasilete madhara kwa watu. Amefafanua kuwa hakuna miundombinu ya maji iliyoathiriwa na mafuriko hayo.

Naye Meneja wa Mamlaka ya Umeme (TANESCO) Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Fadhili Chilombe amesema kuwa wanafuatilia kwa ukaribu madhara yanayoweza kujitokeza kwa kuweka kituo cha dharura (Emergency) maeneo hayo na kuwataka wananchi wa eneo hilo kuwasiliana naye muda wote iwapo kutakuwa na changamoto ya umeme.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa