• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

RC SANARE AAGIZA KUKAMILIKA UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAGUBIKE

Posted on: May 6th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare amewaagiza viongozi wa Wilaya ya Kilosa kukamilisha haraka ujenzi wa jengo la upasuaji la Kituo cha Afya cha Magubike ambalo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliagiza lijengwe na kukamilika ndani ya miezi miwili kuanzia mwezi Machi mwaka huu maagizo yaliyotolewa wakati alipotembelea ujenzi waDaraja la Kiegeya Wilayani Kilosa baada ya kukatika.


Sanare ametoa agizo hilo Mei 5, mwaka huu alipofanya ziara ya siku moja Wilayani humo iliyolenga kusukuma kutekeleza maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyoyatoa Machi 17 mwaka huu alipotembelea ujenzi waDaraja la Kiegeya Wilayani Kilosa baada ya kukatika.

Pamoja na kutoa pongezi kwa viongozi hao katika kutekeleza kwa kiasi kikubwa maagizo ya Mhe Rais, amewaagiza viongozi hao kukamilisha haraka ujenzi wa jengo la upasuaji  la kituo cha Afya cha Magubike ambalo kwa sasa lipo hatua ya upauaji ambapo ametaka Halmashauri kuendelea kutafuta vyanzo mbalimbali ili kukamilisha haraka iwezekanavyo jengo hilo.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale amesema kwa maandalizi ambayo yamekwisha fanyika kusipotokea mabadiliko ujenzi wa jengo hilo utakamilika mwishoni mwa mwezi huu.

Aidha Sanare alitembelea mradi wa maji wa Berega Mgugu ambao unatekelezwa kwa ufadhili wa nchi ya Marekani na kuwapongeza wananchi kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa mradi huo na ametumia fursa hiyo pia kumpongeza mwananchi mmoja Bibi Olivia Chitemo (75) wa Kitongiji cha Gongoni Kijiji cha Belega kwa kujitolea kutoa eneo lake ili lijengwe tenki la maji litakalonufaisha watu zaidi ya elfu tano.  

     

Wakati akikagua utekelezaji wa agizo la Rais la kukarabati daraja la mto Belega Sanare amewapongeza wahandisi waliokuwa wanajenga daraja hilo na kutekeleza kazi hiyo ndani ya siku saba na kusema daraja hilo lina umuhimu wa kipekee kwa kuwa linaunganisha Mikoa mitatu ya Morogoro, Dodoma na Tanga lakini pia limeondoa kero kwa wananchi wanaolitumia kuvuka kwenda Hospitala ya Belega.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wananchi wa Magubike na wanamorogoro kwa jumla kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kwamba ugonjwa wa CORONA kamwe usiwe kisingizio cha wananchi kutoshiriki shughuli za maendeleo, kwani amesema ugonjwa huo haujulikani utakwisha lini na kwamba kinachotakiwa ni kujilinda na kuzingatia maelekezo yanayotolewa na wataalamu wa Afya na Viongozi wa Serikali.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa