• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

SEKTA YA UMMA NA SEKTA BINAFSI ZINATEGEMEANA

Posted on: August 26th, 2020

Sekta ya umma na sekta binafsi ni sekta ambazo zinategemeana hususani katika masuala mbalimbali ikiwemo ukuaji wa shughuli mbalimbali za kiuchumi ambapo Serikali inashughulikia masuala ya kijamii na masuala mengine huku sekta binafsi ikijihusisha zaidi na masuala ya kibiashara.

Hayo yamebainishwa Agosti 26 mwaka huu  na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi wakati akifungua kikao cha baraza la biashara ambapo amesema sekta hizo ni sekta zinazotegemeana na kwamba kutokana na mfumo wa kiuchumi wa nchi ya Tanzania biashara kwa asilimia kubwa zinafanywa sekta binafsi huku Serikali ikifanya masuala makuu ya kijamii na kurahisisha shughuli za kibiashara kufanyika.

Mgoyi amesema kupitia baraza la biashara yapo masuala mbalimbali upande wa Serikali na sekta binafsi yamekuwa na changamoto  lakini kupitia baraza hilo wadau hukutana na kupata mchango mkubwa wa mawazo ambao hupelekea kupata tija kwa maslahi ya pande zote mbili kwani  setkta hizo zinategemeana kwa kiasi kikubwa.

Naye Mtendaji wa chemba ya biashara, viwanda na kilimo Mkoa wa Morogoro Moumin Mwatawala akieleza mwongozo wa baraza la biashara amesema baraza hilo ni jukwaa la rasmi la majadiliano kati ya sekta ya umma na sekta binafsi  linalofanyika katika ngazi ya wilaya. Mkoa na taifa ambapo washiriki wake hutoka pande zote mbili huku akisema kuwa mfumo wa baraza hilo huongozwa na Mkuu wa Wilaya au Mkuu wa Mkoa au Rais kulingana na ngazi ya baraza na kwamba majadiliano huongozwa na mwenyekiti ambaye kwa mujibu wa mwongozo hapaswi kufungamana na upande wowote.

Akitoa taarifa ya mfumo wa upimaji wa wazi wa halmashauri wenye lengo la kuweka mazingira wezeshi upande wa biashara Afisa Biashara Wilaya Idrisa Jukulu amesema mfumo huo unalenga kupima uwezo wa Hamashauri na kuzishindanisha kwa kuzingatia vipimo vya vipengele muhimu 12 ikiwemo kiunzi cha kisheria, ushiriki na mwitikio, mazingira ya kibali, kodi na ada, huduma za mamalaka ya Serikali za Mitaa, huduma za maendeleo ya biashara, miundombinu ya mamlaka ya Serikali za Mitaa, mpango wa matumizi ya ardhi, upataji fedha, uongozi na utawala na jinsia na vijana.


Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa