• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

-Serikali haitosita kulinda Rasilimali watu kwa maslahi ya Maendeleo ya Taifa- Mh. Mhagama

Posted on: December 20th, 2022

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama amesema Serikali ya Awamu ya Sita inatambua mchango mkubwa unaotolewa na watumishi wa umma katika kuwahudumia wananchi na kwani watumishi wa umma ni rasilimali muhimu kwa ustawi wa Taifa.

Hayo yamebainishwa na Mhe. Jenista Mhagama wakati wa ziara yake ya siku moja katika Wilaya ya Kilosa ambapo alizungumza na watumishi lakini pia kutembelea walengwa wa mpango wa kunusuru kaya maskini katika kata ya Mvumi ambapo wakati wa kikao na watumishi wa umma kilicholenga kuhimiza uwajibikaji na kutatua changamoto zinazowakabili watumishi.

Mhe. Jenista amesema kuwa hatomuonea aibu wala huruma kiongozi yeyote aliyepewa dhamana ya kusimamia rasilimaliwatu ambaye atabainika kukiuka sheria na taratibu za usimamizi wa rasilimaliwatu na kuongeza kuwa, viongozi wenye dhamana ya kusimamia rasilimaliwatu wanapaswa kuiheshimu, kuithamini na kuhakikisha inakuwa kwenye mikono salama kwasababu inategemewa na Serikali kwa kiasi kikubwa katika ustawi na maendeleo ya Taifa.

“Rasilimaliwatu ambayo ndio watumishi wa umma ikisimamiwa vizuri itaisaidia Serikali kutimiza lengo la kutoa huduma bora kwa wananchi ikiwa ni pamoja na kutekeleza mipango na mikakati ya maendeleo katika Taifa, na kwamba watumishi wa umma ndio wanategemewa kutoa huduma bora za afya, kuboresha huduma za maji, kuboresha huduma za elimu, kuboresha huduma za miundombinu pamoja na kilimo.” Mhe. Jenista amefafanua.

Kwa upande wa wabunge wa majimbo yote mawili ya Wilaya ya Kilosa Mh. Prof. Palamagamba Kabudi( Kilosa) na Dennis Londo(Mikumi) wameiomba serikali katika utekelezaji wa mpango wa kunusuru Kaya zenye hali duni kutupia jicho maeneo mbalimbali ikiwemoutatuzi wa changamaoto ya kufikika baadhi ya Vijiji vya mpango na hii ni kutokana na kutokuwepo na miundombinu  ya barabara  na vivuko ambavyo si rafiki  hivyo kusababisha shughuli za mpango na uzalishaji kufanyika kwa kiwango kidogo lakini pia utatuzi wa changamoto ya miundombinu ujenzi wa kivuko cha Nyali  pamoja na ukarabati wa barabara inayounganisha Vijiji vya Kigunga, Zombo, Nyali, Madudumizi, Nyameni Zombo na Nyameni yenye urefu wa Kilometa 22.4 ambacho itasaidia kasi ya shughuli za Kilimo cha mazao mbalimbali ili kunufaisha wakazi wapatao 13,485 kufikia huduma ya Afya na Elimu kwa uhakika.  

Pamoja na hayo wameomba uwepo wa ujenzi wa Barabara ya Mkulazi –Tankini yenye urefu wa  Kilometa 6.4 ambayo itasaidia kuwaunganisha wananchi  na shughuli za Kilimo lakini pia ujenzi wa daraja la Nyangara na ukarabati wa barabara yenye urefu wa Kilometa 16  ambayo itaunganisha Vijiji vya Nyangara A na B, Kife na Maguha hii itasaidia kuwaunganisha wananchi na shughuli za uzalishaji wa mazao ya Kilimo na kuweza kufikia huduma za Afya na Elimu wa uhakika.

Akisoma taarifa ya Utekelezaji wa shughuli za mfuko wa maendeleo ya jamii-TASAF katika kijiji cha Mvumi Mtendaji wa Kijiji cha Mvumi Godson Mkasya amesema walengwa wameweza kununua vitu mbalimbali na hivyo kuongeza  mzunguko wa fedha ikiwemo kuweza kulima kwa trekta badala ya majembe ya Mkono, kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi katika Kijiji kama vile kilimo, ufugaji na biashara ndogondogo kwa kupitia ruzuku wanazopokea, wanafunzi 55 toka Kaya za walengwa wananufaika kwa ruzuku ya elimu kwa kupata mahitaji ya msingi, hali ya kiuchumi ya walengwa kuboreka na hivyo kuweza kushiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo pamoja na kuboreka kwa hali ya maisha ya walengwa huku wananchi wakitoa shukrani za dhati kwa Mheshimiwa Rais, Dkt.  Samia Suluhu Hassan na Serikali yake kwa kuendelea kutoa ruzuku za walengwa kupitia Mpango wa kunusuru kaya Lengwa kwani Mpango huu umekuwa mkombozi kwa kaya zenye hali duni kwa Wilaya ya Kilosa.

Akizungumza kwa niaba ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Kilosa, Mwalimu Richard Shagungu ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inayoongozwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kulipa kila mwezi madai ya malimbikizo ya mishahara ya watumishi katika Halmashauri hiyo na kuomba waajiri wasizalishe madai mapya ili Serikali iyamalize madai yaliyopo sasa.


Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa