• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Serikali kuendelea kujiimarisha ili kuboresha mazingira ya wafanyakazi- RC Shigela

Posted on: May 1st, 2022

Katika kuhakikisha mazingira ya watumishi yanaboreshwa kama kupandisha mishahara Serikali ya awamu ya sita chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan Serikali imekuwa ikijiimarisha uchumi kwa kuanzisha miradi ya kimkakati katika miradi itakayofungua fursa za kiuchumi na kuongeza uzalishaji ili Taifa liweze kupata mapato zaidi.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mheshimiwa Martin Shigela wakati wa siku ya Mei Mosi yenye kaulimbiu ‘’Mishahara na Maslahi Bora Kwa Wafanyakazi Ndiyo Kilio Chetu’’#KAZI IENDELEE ambapo amesema Serikali imeendelea kujenga vituo vya afya, shule za sekondari na msingi, hivyo ni dhahiri Serikali inatambua haja na tija kwa wafanyakazi kupata mishahara mizuri na kuboresha mazingira ya kazi ikiwemo upandishaji wa madaraja, na kwamba imetenga bajeti kwa ajili ya kupandisha madaraja watumishi 120,0000 na kulipa malimbikizo zaidi shilingi bilioni 1.3.

Ameelekeza waajiri katika sekta za umma na binafsi kuhakikisha maslahi ya wafanyakazi yanazingatiwa hususani katika uandaaji wa mikataba ya wafanyakazi, kutohamisha watumishi bila kulipwa maslahi stahiki,kutenga bajeti na kutoa fursa sawa za kujiendeleza, kuhakikisha pensheni za wafanyakazi zinapelekwa katika mifuko husika kwa wakati, huku akitoa onyo kwa wasimamizi wa utoaji promosheni kutoa promosheni hizo kwa watumishi stahiki na kwa wakati lakini pia kutozuia wafanyakazi wanapotaka kuanzisha amakujiunga na vyama vya wafanyakazi

Aidha amewasihi wafanyakazi kuwajibika katika maeneo yao kwa kujifanyia tathmini kwa kazi walizofanya, kujituma katika majukumu yao na kuweka mbele suala la ubunifu ili kupata matokeo mazuri katika majukumu yao katika ujenzi wa Taifa ili kupata maendeleo, kwani uzalendo,  kujituma, ubunifu na matokeo ni njia ya kuleta maendeleo sambamba na kuzingatia uadilifu na kuzingatia maadili katika utumishi wa umma.

Nao wabunge wa majimbo ya Kilosa na Mikumi wamewapongeza wafanyakazi wote kwa namna wanavyoihudumia jamii ambapo wamesema maslahi ya wafanyakazi ni jambo la muhimu ili wafanyakazi waweze kufanya kazi kwa ufanisi huku wakisema Serikali ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan imekuwa ikifanyia kazi changamoto mbalimbali za wana Kilosa ikiwemo utatuzi wa kero ya maji, ujenzi wa nyumba za wafanyakazi, ujenzi wa shule ili kupunguza ongezeko la wanafunzi wanaokaa madarasani kwa wingi, ujenzi na ukarabati wa madaraja, Serikali imetoa fedha kwa ajili ya ununuzi wa mashine ya mionzi huku wakisema kuwa zipo promosheni na ajira nyingi zinatarajiwa kutolewa sambamba ongezeko la ajira lakini pia wametaka wananchi kutumia fursa ya uzinduzi wa filamu ya Royal tour kujenga hoteli za viwango ili wageni watakaotembelea hifadhi ya Mikumi kufikia hoteli hizo sambamba na kufufua reli ya Kilosa Mikumi Kidatu ambayo itasafirisha watalii kwa njia ya treni.

Wakieleza kilio chao katika maadhimisho ya siku ya Mei Mosi watumishi hao katika risala yao wameainisha vilio vyao hususani katika Mkoa wa Morogoro ikiwemo wafanyakazi kulipwa mishahara duni kima cha chini kikiwa shilingi 80,000 hadi 100,000, kwa mwezi, kutopandishwa cheo/madaraja kwa wakati, baadhi ya waajiri kutoa mikataba isiyofuata sheria na ya muda mfupi kwa kazi endelevu, utatuzi wa migogoro, ucheleweshaji wa kesi za wafanyakazi zinazosajiliwa Mahakama Kuu Kitengo cha Kazi, matibabu kwa wafanyakazi, malipo ya mikopo ya elimu ya juu.

Changamoto nyingine ikiwa ni kukosa uhuru wa kujiunga na vyama vya wafanyakazi, malipo ya mifuko ya pensheni, ucheleweshaji wa malipo ya kwa wastaafu huku wakiiomba Serikali kuuagiza mfuko wa fidia wa wafanyakazi wanaoumia kazini kulipa wafanyakazi wanaoumia kazini kwa wakati, pamoja na kuutaka mfuko huo kutoa fidia kwa mfanyakazi yoyote anayeumia kazini bila ubaguzi ili mradi mwajiri wake anachangia mfuko huo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa