• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

SERIKALI YADHAMIRIA KUWEKA MKAZO KWENYE VIWANDA VINAVYOZALISHA MALIGHAFI ZA NDANI

Posted on: May 27th, 2020

Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Omary Mgumba mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa kiwanda cha sukari Mkulazi II kilichopo wilayani Kilosa katika kata ya Mbigiri kinachotarajiwa kufungwa mitambo kabla ya mwaka kuisha amewatoa hofu wakulima wadogo na wakati wa miwa kuwa miwa yao haitapotea kwani soko lipo hivyo wasiwe na shaka na mahali pa kuipelekea bidhaa yao ambapo pia amezitaka taasisi za fedha kuendelea kuunga mkono jitihada za kuendeleza mradi huo.

Mgumba amesema Serikali imeadhimia kuongeza mkazo kwenye viwanda vinavyotumia malighafi zinazozalishwa ndani ya nchi ambazo zinatokana na shughuli za kilimo, uvuvi, mifugo, madini na misitu ambapo pia amesema viwanda vyenye soko na mahitaji makubwa ya ndani vitapewa kipaumbele na kiwanda cha sukari ni kimojawapo huku kikifuatiwa na kiwanda cha ngano na mafuta ya kula.

Aidha Naibu Waziri huyo ameishukuru NSSF kwa kufanikiwa kutengeneza barabara ya kutokea Ngerengere mpaka Usungura licha ya changamoto mbalimbali kutokea kama mvua ambayo imeharibu barabara nyingi nchini na kupelekea Serikali kutokuwa na uwezo wa kuzitengeneza zote kwa wakati mmoja lakini pia  amemshukuru mkurugenzi wa TARURA kwa kutoa milioni mia mbili kwa ajili ya matengenezo ya  barabara ya kutokea Ngerengere mpaka katika shamba la Mkulazi.

Akijibu swali la Naibu Waziri juu ya soko kwa upande wa miwa ambayo ipo tayari kwa matumizi Mtendaji Mkuu wa Mkulazi Selestine Some amesema ununuzi wa miwa ambayo ipo tayari kiwanda cha sukari cha Mtibwa kimeanza kununua miwa kwa wakulima hao licha ya malalamiko ya bei ya kuuza miwa hiyo ambapo mkataba wa awali ulisema miwa itauzwa kwa shilingi 80,000 kwa tani huku Mtibwa wakinunua kwa 60000 kwa tani hii ni kutokana na changamoto za kuchelewa kwa mradi huo na barabara za kwenda shambani kutokupitika ambapo iliwalazimu Mkulazi kuongea na benki ya Azania kusitisha riba ya mkopo uliotolewa kwa wakulima na kukubaliana marejesho kuanza kufanyika mwaka 2021.

Pamoja na hayo Mkurugenzi Mkuu wa NSSF William E. Erio amesema NSSF wanafanya uwekezaji ambao lazima ulete tija na kwamba uwekezaji wa NSSF unafanyika chini ya miongozo ya Benki Kuu ambapo pia ameomba kuwepo kwa elimu kwa wakulima juu ya mikataba inayofanyika ili waweze kuwa na uelewa wa pamoja kwa kuangalia mikataba inajazwa kwa kuzingatia vigezo vya ubora wa bidhaa lakini pia iwepo elimu ya namna ya uzalishaji ili bidhaa zizalishwe kulingana na mahitaji ya viwanda.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi amesisitiza kuwa taarifa za muhimu kuhusu maendeleo ya mradi wa kiwanda cha sukari cha Mkulazi ziwe zinatolewa kwa wakulima ili kuwaondoa hofu kwa kuonyesha jitihada zinazofanyika kwa ajili ya kukamilisha mradi huo, huku Mkurugezi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale akiongeza kusema jitihada zinazofanyika katika kuendeleza mradi huo zifanyike pia katika kutengeneza miundombinu ili eneo la mradi huo liweze kufikika kwa urahisi.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa