• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Shilingi bilioni 1.1 kujenga daraja mto Ruhembe

Posted on: January 29th, 2022

Kati ya mwaka 2019 na 2021 watu 26 wamepoteza maisha wakati wakivuka katika mto Ruhembe kwa kusombwa na maji katika kipindi cha mvua za masika kutokana na eneo hilo kukosekana kwa darajamkatika eneo hilo ambapo kufuatia tukio hilo Serikali imepeleka zaidi ya shilingi bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa daraja lenye urefu wa mita 40 la mto Ruhembe hivyo kukamilika kwake utakua mwarobaini wa changamoto hiyo.

Akizungumza katika hafla ya mkandarasi Fomast Campany limited kukabidhiwa eneo la mradi wa ujenzi wa daraja hilo Diwani wa kata ya Ruhembe, Salum Mponzi amesema kumalizika kwa ujenzi wa daraja hilo itakuwa faraja kwa wakazi wa kata nne za Kidodi, Ruhembe, Ruaha na Vidunda kutokana na jamii za wananchi hao kutegemeana katika mahitaji mbalimbali.

Mponzi amesema ana amini daraja hilo litakuwa mkombozi kwa wananchi wa kata hizo ambazo wanategemeana zaidi katika shughuli za kilimo na mahitaji mbalimbali huku akisema kuwa kazi iliyopo mbele yao ni kushirikiana na mkandarasi katika kutunza vifaa pindi vitakapoletwa na kuwa wananchi wa maeneo hayo watafaidika na mradi huo Wakati wananchi wakiweka matumaini ya daraja hilo ili kuwaondoa adha wanazopata,


Wakati wananchi wakiweka matumaini ya daraja hilo ili kuwaondoa katika adha wanazopata, Mkuu wa wilaya ya Kilosa, Alhaji Majid Mwanga ametumia nafasi hiyo kuwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa mkandarasi lakini huku akiwaonya wazazi ambao hawajawaapeleka shule watoto kwa visingizio mbalimbali kuchukua hatua za dhati na kuwapeleka shule watoto hao ili wapate haki ya elimu huku Mbunge wa jimbo la Mikumi Mh. Dennis Londo akisema Serikali sikivu ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan baada ya kusikia kilio cha wakazi wa Ruhembe inatenga zaidi ya shilingi bilioni moja na kumkabidhi mkandarasi ili kufikia mwezi June 2022 wananchi wa kata hiyo wawe wanapita juu ya daraja na hivyo kunusuru maisha yao

Naye Meneja wa Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini Wilaya ya Kilosa (Tarura), Mhandisi Harold Sawaki amesema mradi huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 1.1 na daraja hilo litakuwa na urefu wa mita 40 huku likitarajiwa kukamilika katika kipindi cha miezi mitano kuanzia muda waliosainiana na mkandarasi huku Meneja wa kampuni ya Fomast Campany limited Dar es Salaam, Hanaf Mbaruku akitaka wananchi na viongozi kutoa ushirikiano mkubwa wakati wote wa mradi huo lakini kujiepusha na matukio ya wizi wa vifaa kwani itakuwa kukwamisha kazi isimalizike kwa wakati.

Kwa niaba ya wakazi wa kijiji cha Ruhembe, Mwalimu Rose Mremba amesema kuwa nyakati za masika wamekuwa wakitumia fedha nyingi kati ya sh5,000 hadi sh10,000 kufika upande wa pili kama gharama za usafiri ambapo maji yakiwa kidogo kiasi mtoni utavushwa kwa sh5,000 kwa kubebwa mgongoni lakini yakijaa utaweza kukodi usafiri hadi sh10,000.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa