• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

SHIRIKISHENI VIONGOZI WA SERIKALI ZA VIJIJI KUTATUA CHANGAMOTO ZA KAMBI

Posted on: August 20th, 2019

Katibu Tawala Wilaya Yohana Kasitila ametoa wito kwa wakuu wa shule mbalimbali zilizoweka kambi kwa ajili ya maandalizi ya mitihani ya kidato cha nne 2019 kushirikisha viongozi wa serikali za vijiji  sambamba na  jamii inayowazunguka katika utatuzi wa changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika uendeshaji wa kambi hizo hususani suala la uchangiaji wa chakula kwa ajili ya watoto hao.

Kasitila amesema hayo Agosti 19/08/2019 wakati alipotembelea shule za sekondari zilizopo tarafa ya Mikumi na Ulaya ikiwemo kambi ya Masanze inayojumuisha shule za Mati Tindiga, Masanze, Zombo na Kilangali huku shule nyingine zilizotembelewa ni Mikumi, Iwemba na Kidodi ambapo miongoni mwa changamoto zilizobainishwa ni upungufu wa chakula ambacho kinachangiwa na wazazi wa watoto husika

Kasitila amesema kuwa viongozi wa serikali za vijiji wakishirikishwa kikamilifu hamasa ya uchangiaji itakuwa kubwa ikiwemo kupata michango toka katika misikiti na makanisa kupitia viongozi wa dini sambamba na kuwashirikiasha wafanyabiashara na taasisi mbalimbali.

Aidha amezitaka shule ambazo bado hazijaanza kambi kuanza kambi hizo mara moja ambapo agizo lilitolewa na Mkuu wa Wilaya kuanza kambi hizo tarehe 01/8/2019 lengo ikiwa ni kufikia malengo ya wilaya kufuta daraja ziro na daraja la nne ambapo kupitia kambi hizo zitakazokuwa zikifundishwa na walimu mahiri zitaleta matokeo chanya na kuongeza kiwango cha ufaulu .

Pamoja na hayo ameendelea kuwakumbusha walimu katika kambi zote kuhakikisha wanaweka utaratibu wa kujipima kile wanachowekeza kwa wanafunzi kwa kutoa majaribio na mitihani ili kuona uelewa wa wanafunzi hao sambamba na kuona matokeo ya uwepo wa kambi hizo.

Pamoja na hayo   ametoa kwa wanafunzi wa kidato cha nne kutumia vema fursa za uwepo wa kambi hizo kusoma kwa bidiii ili kupata matokeo tarajiwa ya ufaulupamoja na kufuta daraja ziro na la nne  ambayo yatawasaidia kuendelea na kidato cha tano sambamba na kuwa na maisha mazuri hapo baadae

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa