• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WANAFUNZI WABUNIFU WA SHULE YA MSINGI MIKUMI MPYA WAPATIWA ZAWADI

Posted on: March 7th, 2024

Shule ya Msingi Mikumi mpya iliyopo Kata ya Mikumi  Wilayani Kilosa imekabidhi zawadi kwa watoto wabunifu wa Vitu mbalimbali vya kisayansi ikiwa ni mwendelezo wa uibuaji wa vipaji kwa vijana wabunifu wanaosoma shuleni hapo ili kukuza ubunifu wao siku za usoni.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi zawadi kwa washindi iliyofanyika Machi 7,2024 Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Ibrahimu Chembe amesema kuwa shule hiyo imepokea kiasi cha Shilingi milioni 1 kwaajili ya kukuza na kuendeleza ubunifu pia uandaaji wa karakana itakayokuwa na vifaa mbalimbali vitakavyosaidia  wanafunzi katika suala ubunifu.

Fedha hizo zimetolewa na Tume ya Sayansi na teknolojia (COSTEC) kufuatia Shule hiyo kutoa mshindi wa kwanza kitaifa wa Mashindano ya Ubunifu kwa watoto upande wa shule za Msingi (MAKISATU) kwa mwaka 2022, yaliyoandaliwa na tume hiyo.

Mwalimu Chembe ameongeza  kuwa  tayari mikakati ya uibuaji na uendelezaji wa vipaji vya ubunifu shuleni hapo unaendelea ambapo mwaka 2023 mwezi Novemba shule iliandaa mashindano kwa wanafunzi ambapo takribani wanafunzi 8 walishiriki na baada ya kuchujwa wamepatikana washidi watatu,Sambamba na hayo amewapongeza washindi hao na kuwataka kuendeleza vipaji vyao ili waweze kufanya vizuri zaidi na kuendeleza vipaji vyao.

Kwa upande wake Afisa Elimu ya Awali na Msingi Bi. Zakia Fandey amesema kuwa huo ni mwanzo tu na kwamba suala hilo litaendelea kufanyika shuleni hapo na amewataka wanafunzi kuendelea kubuni kazi mbalimbali za ubunifu kwani fursa iko wazi kwa kila mwanafunzi.

Aidha amesema kuwa Wilaya itaendelea kupatanua wigo ili shule nyingi zaidi  kutoka Kata zote 40 Wilayani hapa ziweze kushiriki kwani anaamini kuna watoto wengi wenye vipaji vya kubuni kazi mbalimbali za kisayansi na kwamba kama watapata nafasi na watu wa kuwaongoza na kuwaelekeza kuna fursa ya kupata kazi nyingine kubwa zaidi ya awali.

Amewataka Walimu kutoa elimu shirikishi kwa kuwapa wanafunzi nafasi ya kueleza wanachokijua kwani watoto wanavitu vikubwa na vizuri hivyo ili kuviona ni lazima walimu waweze kuibua vipaji na kuwa tayari kufundisha kwa vitendo.

Ameongeza  wana mpango wa kuandika andiko lingine la kuomba fedha ili kutanua wigo wa ubunifu hivyo amewataka walimu kuwaandaa wanafunzi mapema ili ikifika muda wa mashindano ya ubunifu wanafunzi wawe tayari wameshaandaliwa.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa