• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

SIMAMIENI RASILIMALI ZA UMMA IPASAVYO

Posted on: December 3rd, 2018

Katibu Tawala Wilaya ya Kilosa Yohana Kasitila ametoa rai kwa waheshimiwa madiwani na watendaji wa kata kuwa mstari wa mbele kukemea mapungufu mbalimbali yanayojitokeza katika usimamizi wa miradi na rasilimali za umma kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia miradi na rasilimali hizo kutunzwa ipasavyo ili kuweza kufaa kwa matumizi ya kizazi cha sasa na kijacho.

Rai hiyo imetolewa wakati wa kikao kilichoandaliwa na taasisi ya Dira Theatre kilichohusu mrejesho wa utekelezaji wa mradi wa wajibu wa jamii na viongozi katika kufuatilia na kusimamia matumizi ya rasilimali za umma katika sekta ya elimu ambapo amesema kuwa viongozi wanayo nafasi kubwa katika kuhamasisha jamii na kuhakikisha wananchi wanashiriki kwa kiwango kikubwa kutunza rasilimali hizo ambazo wao ndio wahusika wakuu kuona zinapatikana na zinatumika ipasavyo katika maeneo yao.

Kasilila amesema kuwa madiwani na watendaji wa kata wanao wajibu wa kuhakikisha mikutano na vikao vya kisheria vinafanyika ipasavyo kwani kupitia vikao hivyo vinavyohusisha wananchi vitatoa fursa kwa wananchi hao kujua kinachoendelea na ushiriki wao kwani kwa kufanya hivyo itasaidia kwa kiasi kikubwa uwepo wa maendeleo kiujumla ikiwemo katika sekta ya elimu.

Akijibu swali kutoka kwa waandishi wa habari waliohudhuria kikao hicho kuhusu kushuka kwa kiwango cha ufaulu wilayani Kilosa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Lucas Mwambambale amesema kiwango cha ufaulu hakijashuka bali kimepanda kwani ufaulu umepanda kutoka 59% hadi 63% na kwamba licha ya ukubwa wa Wilaya na wingi wa shule, upungufu wa walimu, masuala ya mila na desturi na changamoto nyinginezo Halmashauri imejiwekea mipango madhubuti ya kuongeza kiwango cha ufaulu na elimu kwa ujumla na kwamba kwa sasa ofisi yake imepeleka ombi Ofisi ya Rais kuongeza nguvu katika umaliziaji wa majengo ya madarasa pamoja na kukabiliana na upungufu wa vyumba vya madarasa, viti na madawati.

Naye Mkurugenzi wa taasisi ya Dira Theatre Erasmo Tullo amesema mradi huo unafanya kazi katika kata za Zombo, Masanze, Mabwerebwere, Mabula, Mbumi, Mtumbatu, Mkwatani, Lumbiji, Kilangali, Tindiga, Ulaya, Kasiki, Magomeni na Mamboya lengo ikiwa ni ufuatiliaji wa rasilimali za umma ni kuweka bayana matumizi sahihi ya rasilimali za umma, kuboresha hali ya utoaji huduma upande wa elimu na kukuza uwajibikaji jambo ambalo litasaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza ufanisi katika utendaji kazi pamoja na nidhamu ya matumizi ya rasilimali hizo.

 

                                   

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa