• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

TASAF KUFANYA UHAKIKI WA KAYA ZA WALENGWA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI

Posted on: July 20th, 2020

Kupitia utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini wawezeshaji wa Halmashauri kuhusu utekelezaji wa kipindi cha pili cha awamu ya tatu ya TASAF na uhakiki wa kaya za walengwa wa Mpango wa Kunusuru kaya Maskini wametakiwa kuzingatia misingi ya uadilifu katika kazi yao na kutotumia fursa hiyo kwa kutengeneza mazingira ya rushwa.

Rai hiyo imetolewa Julai 20 mwaka huu na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha wawezeshaji hao ambapo amewataka kuzingatia misingi ya uadilifu katika utendaji kazi kwa kutenda haki na kuzingatia misingi ya utumishi wa umma.

Mwambambale amesema katika eneo la uwajibikaji na uadilifu katika zoezi hilo la uhakiki ni vema kazi ikafanyika vizuri kwani kazi hiyo inahitaji umakini, weledi na upembuzi yakinifu ili kutoaji haki kwa kadri inavyostaki.

Naye Afisa Program wa TASAF Karim Kondo akisoma hotuba kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF amesema tathmini ya utekelezaji wa kipindi cha kwanza cha awamu ya tatu ya TASAF inaonyesha mpango wa kunusuru kaya maskini nchini umechangia kwa kiasi kufikiwa azma ya Serikali ya kupunguza umaskini wa mahitaji ya msingi kwa kaya kwa 10% na umaskini uliokithiri umepungua kwa 12% kwa kaya maskini nchini.

Kondo amesema katika kipindi cha pili cha awamu ya tatu ya mfuko wa TASAF III kitatekelezwa katika Halmashauri zote 185 za Tanzania Bara na wilaya zote za Zanzibar na kujumuisha maeneo ambayo hayakupata fursa katika kipindi cha kwanza cha utekelezaji ambacho kimekamilika  mkazo mkubwa ukiwa katika kuwezesha kaya zitakazoandikishwa kwenye mpango wa kufanya kazi ili kuongeza kipato.

Mwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye pia ni Afisa Ufatiliaji TASAF Bi.  Simth Haule amesema madhumuni ya Mpango katika kipindi cha pili ni kuwezesha kaya za walengwa kutumia fursa za kuongeza kipato na huduma za jamii na uchumi na kuwekeza katika kuendeleza watoto wao huku msisitizo ukiwa katika kuwezesha kaya kufanya kazi ili kuongeza kipato, kuwezesha kaya kuongeza rasilimali zalishi na vitega uchumi, kuwekeza katika rasilimali watu hususan watoto ili kuleta matokeo chanya yatakayodumu kwa muda mrefu, kuboresha upatikanaji wa huduma za maji, afya na elimu pamoja na kukuza uchumi wa eneo unakofanyika utekelezaji kutokana na matokeo ya Mpango.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa