• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

TASAF yatoa mwongozo kwa madiwani juu ya mpango wa kuweka akiba na kukuza uchumi wa kaya

Posted on: May 9th, 2018

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa ikitekeleza Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) tangu mwaka 2000 lengo likiwa ni kuongeza kipato, fursa na kuongeza uwezo wa kugharamia mahitaji mengine ya kaya za walengwa kupitia utekelezaji wa sehemu kuu nne za mpango huo.

Akieleza sehemu hizo za mpango huo wa TASAF Mei 08 2018 Afisa Mafunzo na Ushirikishwaji Catherine Kisanga wakati akitoa mafunzo kwa  kwa waheshimiwa madiwani wa Wilaya ya Kilosa amesema kuwa sehemu hizo ni uhawilishaji fedha na ajira za muda, mpango wa kuweka akiba na kukuza uchumi, kuboresha miundombinu na kujenga uweza katika ngazi mbalimbali za utekelezaji.

Lengo la Mpango Kuweka Akiba ni kuongeza uwezo wa kuzalisha kipato cha kaya ili walengwa waweze kujisimamia wenyewe kwa vipindi vya kati na muda mrefu kwa kuwajengea uwezo wa uzalishaji hatua kwa hatua za kujitegemea kiuchumi kwa kaya na kuongeza vyanzo vya kipato,kwani unachangia ujenzi wa msingi wa kutoka kwenye umaskini kwa kuongeza uwezo wa kaya kujisimamia na kuimarisha kipato kupitia vyanzo mbalimbali ikiwemo kilimo, mifugo,biashara na kazi za ujira.

Akieleza ni namna gani mpango huo utafanyika amesema walengwa watapata elimu kuhusu stadi za maisha usimamizi wa bajeti ya kaya pia watafahamishwa fusra za mpango, jinsi ya kupata huduma za ugani, kuzalisha kwa tija, jinsi ya kupata masoko na kuongeza thamani.

Sambamba na hayo walengwa watahamasishwa kujiunga kwenye vikundi vya akiba na kuwa malengo yenye tija huku wakipata maelezo na habari mbalimbali za mambo yanayokidhi mahitaji yao kama vile ruzuku za mitaji ili kukuza na kuendesha miradi ya kuzalisha kipato kwa kaya.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri Mheshimiwa Hassan Mkopi kwa niaba ya madiwani wote licha ya kuishukuru TASAF kwa kuwajengea uelewa juu ya mpango huo, amewataka madiwani wenzake kushiriki kikamilifu katika kata zao kusimamia mpango huo kwa kuhakikisha walengwa wanafikiwa na kupata huduma stahiki hatimaye kuinuka kiuchumi na kufikia malengo ya millennia.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa