• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

TOENI USHIRIKIANO KWA WADAU WANAOFANYA KAZI NA KILOSA

Posted on: July 10th, 2020

Wananchi wilayani Kilosa wametakiwa kuendelea kutoa ushirikiano kwa wadau mbalimbali wanaoonyesha nia ya kufanya kazi na wilaya ya Kilosa kwa lengo la kuleta maendeleo hususani katika shughuli za miradi mbalimbali ya maendeleo kwani miradi hiyo ni kwa faida ya wananchi na vizazi vyao.

Rai hiyo imetolewa Julai 16 mwaka huu na Mtendaji wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kilosa Reginald Samba aliyekuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Katibu Tawala Wilaya katika hafla ya makabidhiano ya majukumu ya uendeshaji mradi wa maji katika vijiji vya Mandela, Magole A na B vilivyopo katika kata ya Magole miradi ambayo imefadhiliwa na shirika lisilokuwa la kiserikali WARIDI ambalo linafadhiliwa na watu wa Marekani(USAID) kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya kupitia ofisi ya RUWASA.

Simba amesema kuwa miradi huo wa  WARIDI ni mradi unaoshughulika na kusaidia jamiii kupata maji safi na salama na kuboresha huduma ya maji ndani ya jamii ambapo kupitia miradi hiyo itapunguza kero ya maji kwa 90%, itaongeza  makusanyo ya maji na kuendesha chombo cha watumia maji, kupata elimu ya ujasiriamali jambo litakalosaidia kukuza uchumi kwa wananchi lakini pia kuongezeka kwa shughuli mbalimbali zinazotumia maji ikiwemo ufyatuaji tofali, bustani ndogo ndogo na kukuza uchumi wa vijiji hivyo.

Pamoja na hayo Simba ameitaka RUWASA kuhakikisha inazifanyia kazi changamoto mbalimbali zilizobainishwa na wananchi ikiwemo kuhakikisha wanafunga mita kwa wateja wa majumbani, kuhakikisha maeneo ambayo bado maji hayajafika yaweze kufikiwa, kujenga uelewa kwa wananchi namna ya utendaji kazi na utunzaji miundombinu ya maji lakini pia kuunda jumuiya ya watumia maji huku akitoa onyo kwa kwa wanajiunganishia maji kinyume cha taratibu.

Kwa upande wa gharama zilizotumika katika kutekeleza miradi hiyo ya maji kwa vijiji vya Mandela A na B ni shilingi 418,764,927.6 huku kijiji cha Mandela ukigharimu shilingi 379,875,068.26 ambapo katika makabidhiano hayo WARIDI imekabidhi michoro ya ujenzi pamoja na nyaraka zinazohitajika kwa Halmasharui na  RUWASA.

Akieleza namna WARIDI inavyofanya kazi Mkuu wa Mradi Bigambo Nandiga amesema kwa asilimia kubwa WARIDI inafanya kazi na Mkoa wa Morogoro ambapo wamefanya shughuli mbalimbali katika maeneo mbalimbali ambapo katika Wilaya ya Kilosa licha ya miradi ya maji lakini pia imesaidia ujenzi wa vyoo katika shule tano zilizopo wilayani Kilosa lakini pia amesisitiza kuendelea kutunzwa kwa miradi hiyo kwa faida ya vizazi vijavyo ili idumu na kutoa matokeo tarajiwa.

Akizungumzia upatikanaji wa maji Meneja RUWASA Wilaya Injinia Josh Chum amesema RUWASA inatekeleza miradi ya maji maeneo mengi na kwamba hadi kufikia Disemba 2019 upatikanaji maji vijijini ilifikia 73% huku miji midogo ikiwa 85%  na kwamba kwa kiwango kikubwa ukanda wa mikumi maeneo mengi yana maji ambapo kwa sasa kupitia ushirikiano wa WARIDI wapo katika ukanda wa tarafa ya Magole ambapo vinategemewa kuchimbwa visima 18 japokuwa ukanda huo una shida ya upatikanaji wa maji.

Aidha amesema zipo changamoto katika utekelezaji wa miradi hiyo ikiwemo usimamizi wa miradi, utekelezaji wa miradi kulingana na utaratibu unaotolewa na wadau ambapo pia amesema wamejipanga kuhakikisha maeneo yote ambayo hayana jumuia za watumia maji yanakuwa na jumuiya za watumia maji huku akiwashukuru wananchi kiujumla kwa ushirikiano walioutoa katika utekelezaji wa miradi hiyo ikiwemo kuchangia nguvu kazi katika miradi hiyo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa