• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

TUSHIRIKIANE KUTOA ELIMU YA AFYA YA UZAZI NA MTOTO - DC KILOSA

Posted on: September 24th, 2018

Imeelezwa kuwa viongozi wa dini na siasa wanayo nafasi kuwa ya kuhamasisha jamii kuhakikisha kina mama wajawazito wanajifungulia katika vituo vya kutolea huduma badala ya kuendelea kujifungulia kwa wakunga wa jadi au majumbani lengo ikiwa ni kupunguza vifo vya akina mama na watoto chini ya miaka mitano pamoja na kuiimarisha jamii kuwa na afya bora ya uzazi na mtoto.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi wakati  wa kikao kilichohusisha viongozi wa dini na siasa ambapo amesema kuwa viongozi hao wano wajibu kuelimisha walio chini yao hasa wanaume kuthamini afya za wenza wao kwani serikali kwa upande wake inajitahidi kuhakikisha huduma husika zinapatikana hivyo viongozi wa dini na siasa licha ya kuongea masuala ya kidini lakini pia watumie majukwaa yao kuzungumzia elimu ya afya uzazi na mtoto.

Naye Mratibu wa Huduma za Afya ya Uzazi na Mtoto Wilaya ya Kilosa Sophia Mpunga amesema kuwa kitengo cha huduma za afya ya uzazi na mtoto kinatoa huduma ya upimaji wa wajawazito na maendeleo ya ukuaji wa mimba ambapo licha ya huduma hizo wamekuwa wakikumbana na changamoto  zinazosababisha vifo kwa mama na mtoto ikiwemo kuchelewa kuanza kliniki, mahudhurio hafifu ya wenza wakati wa kuanza kliniki, uelewa mdogo kwa jamii kuhusu huduma za afya ya uzazi na mtoto hasa uzazi wa mpango na tatizo la kujifungulia nyumbani na kwa wakunga wa jadi.

Aidha kikao hicho kilipata fursa ya kujadiliana namna ya kuweka mikakati ya kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kutoka watu 16 hadi kufikia 10 kwa mwaka ambapo Mhe. Daud Mfaume diwani wa kata ya Kasiki na Mhe Yahaya Mwinchea diwani wa kata ya Mkwatani wametoa rai kuendelea kuhamasisha jamii kutumia njia salama za uzazi na kuzuia vifo  pamoja na kupata takwimu sahihi ili kupunguza vifo na kushauri watu waende hospitali na wanaume kuacha kauli zisizofaa pindi inapohitajika kwenda kiliniki na wenza wao.

Nao viongozi wa dini kwa pamoja wameahidi kutumia misikiti na makanisa kuelezea waumini wao juu ya uzazi na kuachana na tabia za usiri lakini pia wametoa wito kwa wahudumu wa afya kuwa na kauli nzuri na upendo wanapopokea wagonjwa hali ambayo inatawahamasisha kina mama kujifungulia vituo vya kutolea huduma badala ya kukimbilia kwa wakunga wa jadi.

Naye Afisa Ustawi wa Jamii Bi. Tumaini Geugeu kwa niaba ya Mganga Mkuu Wilaya amesema licha ya sababu mbalimbali zinazosababisha vifo kwa mama na mtoto mimba za utotoni na ndoa ambazo sio rasmi ni miongoni mwa vyanzo vya vifo hivyo kwani zina madhara meengi ikiwemo ukatili, kubakwa, usiri katika kutoa elimu kwa watoto ili waweze kujitambua na kutokomeza mimba za utotoni.

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 KWA SHULE ZA SEKONDARI HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOSA July 14, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI September 16, 2023
  • ZABUNI January 31, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • KILOSA KUDUMISHA USAFI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    September 20, 2023
  • TIMU YA UKAGUZI MKOA YATEMBELEA MIRADI YA BOOST KILOSA

    September 20, 2023
  • MAPATO YA HALMASHAURI YAONGEZEKA KUTOKA ASILIMIA 94 MPAKA ASILIMIA 98.91

    September 01, 2023
  • Walimu watakiwa kuendelea kuzifahamu huduma za kibenki

    August 29, 2023
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa