• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

TUSHIRIKIANE KUTOA ELIMU YA AFYA YA UZAZI NA MTOTO - DC KILOSA

Posted on: September 24th, 2018

Imeelezwa kuwa viongozi wa dini na siasa wanayo nafasi kuwa ya kuhamasisha jamii kuhakikisha kina mama wajawazito wanajifungulia katika vituo vya kutolea huduma badala ya kuendelea kujifungulia kwa wakunga wa jadi au majumbani lengo ikiwa ni kupunguza vifo vya akina mama na watoto chini ya miaka mitano pamoja na kuiimarisha jamii kuwa na afya bora ya uzazi na mtoto.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi wakati  wa kikao kilichohusisha viongozi wa dini na siasa ambapo amesema kuwa viongozi hao wano wajibu kuelimisha walio chini yao hasa wanaume kuthamini afya za wenza wao kwani serikali kwa upande wake inajitahidi kuhakikisha huduma husika zinapatikana hivyo viongozi wa dini na siasa licha ya kuongea masuala ya kidini lakini pia watumie majukwaa yao kuzungumzia elimu ya afya uzazi na mtoto.

Naye Mratibu wa Huduma za Afya ya Uzazi na Mtoto Wilaya ya Kilosa Sophia Mpunga amesema kuwa kitengo cha huduma za afya ya uzazi na mtoto kinatoa huduma ya upimaji wa wajawazito na maendeleo ya ukuaji wa mimba ambapo licha ya huduma hizo wamekuwa wakikumbana na changamoto  zinazosababisha vifo kwa mama na mtoto ikiwemo kuchelewa kuanza kliniki, mahudhurio hafifu ya wenza wakati wa kuanza kliniki, uelewa mdogo kwa jamii kuhusu huduma za afya ya uzazi na mtoto hasa uzazi wa mpango na tatizo la kujifungulia nyumbani na kwa wakunga wa jadi.

Aidha kikao hicho kilipata fursa ya kujadiliana namna ya kuweka mikakati ya kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kutoka watu 16 hadi kufikia 10 kwa mwaka ambapo Mhe. Daud Mfaume diwani wa kata ya Kasiki na Mhe Yahaya Mwinchea diwani wa kata ya Mkwatani wametoa rai kuendelea kuhamasisha jamii kutumia njia salama za uzazi na kuzuia vifo  pamoja na kupata takwimu sahihi ili kupunguza vifo na kushauri watu waende hospitali na wanaume kuacha kauli zisizofaa pindi inapohitajika kwenda kiliniki na wenza wao.

Nao viongozi wa dini kwa pamoja wameahidi kutumia misikiti na makanisa kuelezea waumini wao juu ya uzazi na kuachana na tabia za usiri lakini pia wametoa wito kwa wahudumu wa afya kuwa na kauli nzuri na upendo wanapopokea wagonjwa hali ambayo inatawahamasisha kina mama kujifungulia vituo vya kutolea huduma badala ya kukimbilia kwa wakunga wa jadi.

Naye Afisa Ustawi wa Jamii Bi. Tumaini Geugeu kwa niaba ya Mganga Mkuu Wilaya amesema licha ya sababu mbalimbali zinazosababisha vifo kwa mama na mtoto mimba za utotoni na ndoa ambazo sio rasmi ni miongoni mwa vyanzo vya vifo hivyo kwani zina madhara meengi ikiwemo ukatili, kubakwa, usiri katika kutoa elimu kwa watoto ili waweze kujitambua na kutokomeza mimba za utotoni.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI KILOSA DC June 06, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • DC SHAKA AWATAKA VIONGOZI WA VIJIJI KUCHUKUA HATUA DHIDI YA VITENDO VYA UVUNJIFU WA AMANI KIDUHI

    June 19, 2025
  • DC SHAKA AWATAKA VIONGOZI NGAZI YA KATA NA VIJIJI KUSIMAMIA NA KUFUATILIA MIRADI YA MAENDELEO IPASAVYO

    June 19, 2025
  • DC SHAKA AWATAKA WAZAZI / WALEZI KUWAJIBIKA KATIKA MALEZI BORA YA WATOTO

    June 16, 2025
  • TIMU YA MENEJIMENTI KILOSA YAFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    June 12, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa