• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Ubalozi wa Switzerland kuendelea kutoa ushirikiano kwa Kilosa ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi

Posted on: December 7th, 2023

Serikali ya Switzerland imeendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kupunguza madhara yatokanayo na mabadikliko ya tabia kupitia program mbalimbali kwa vijana kufanya shughuli rafiki kwa mazingira ikiwemo upandaji miti ya kutosha ambayo itakuwa ikipandwa katika maeneo mbalimbali yatakayotengwa kwa ngazi ya vijiji.

Hayo yamebainishwa mwanzoni mwa wiki hii na Mkuu wa Sehemu ya Ajira na Mapato ubalozi wa Switzerland nchini Tanzania Bw.Peter Sidler  wakati wa uzinduzi wa kampeni ya vijana ya upanndaji miti ambapo amesema uwepo wa miti ya kutosha utasaidia kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi lakini pia miti hiyo ya aina mbalimbali miti maji, mizambarau na mingineyo itasaida kupunguza athari za mafuriko lakini pia itasaidia shughuli mbalimbali ndani ya vijiji ikiwemo ujenzi wa ofisi za vijiji, upatikanaji wa samani mbalimbali ambazo zinaweza kutumika shuleni, vituo vya afya na zahanati

Mratibu wa Mtandao wa Vikundi vya Wakulima na Wafugaji Morogoro(MVIWAMORO) Joseph Sengasenga amesema kapitia kampeni ya youth green MVIWAMORO imetoa miche ya miti 5000 kwa kata za Rudewa kwa kijiji cha Rudewa Gongoni na Mvumi ambapo kila kata imepata miche ya miti 2500 ambayo inapandwa katika maeneo ya mikakati ikiwemo maeneo ya nyumba za ibada, ofisi za watendaji wa vijiji na kata, shule za msingi na sekondari, vituo vya afya na zahanati pamoja na maeneo ya taasisi zilizopo katika vijiji husika. 

 Sengasenga amesema pamoja na ugawaji  wa miti pia wametoa elimu kwa vijana 50 juu ya utunzaji wa mazingira na ufundi stadi elimu ambayo itawasaidia namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kwamba kupitia upandaji miti ya aina mbalimbali itasaidia kutunza mazingira, kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi lakini pia vijana hao watapata miche ya miti ambayo watapanda maeneo malimbali kwa lengo la kujiongezea kipato kupitia miti ya mbao na matunda.

Kwa upande wake Afisa Mazingira Amal Shebe amesema upatikanaji wa miche ya miti 5000 kwa kata ya Rudewa na Mvumi itasaidia kwa kiasi kikubwa kupandwa kwenye kingo za maji hivyo kupelekea kupungua kwa adha ya mafuriko, kwani maeneo mengi ni hatarishi na hayafikiki kwa urahisi kwani kijiografia maeneo mengi ya Kilosa yapo chini hivyo kingo za maji zinashindwa kuhimili maji yanayotoka maeneo ya juu na kwamba Halmashauri inaendelea na jitihada za kupanda miti kwa wingi ili kuepuka madhara ya mafuriko.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa