• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

UHAKIKI WA MASHAMBA YALIYOFUTWA KUFANYIKA UPYA- LUKUVI

Posted on: May 16th, 2019

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh William Lukuvi ameitaka jamii na wananchi kwa ujumla kutambua kuwa lengo la kufuta mashamba ambayo serikali imekuwa ikiendelea kuyafuta ni kutoendelezwa na wanaoyamiki hali ambayo inasababisha wananchi kukosa mashamba ya kulima kwa ajili ya kujikimu kimaisha na kujiongezea kipato.

Lukuvi amesema hayo Mei 16 katika ziara yake wilayani Kilosa na kusema kuwa lengo la ziara yake ni kuitambulisha rasmi timu ya uhakiki wa mashamba yaliyofutwa ambapo timu hiyo itafanya upya uhakiki upya wa mashamba yote yaliyofutwa, historia ya mashamba hayo lengo ikiwa ni kupata uhalali wa wamiliki wa maeneo hayo pamoja na kutoa mapendekezo ya mgawanyo kwa kuangalia wananchi wote wenye uhitaji ili kufanya uhalali ambapo ardhi nyingine itatengwa kwa ajili ya uwekezaji ili kutengeneza mazingira ya uwekezaji na upatikanaji wa ajira kwa wananchi wa wilaya ya Kilosa na Mkoa wa Morogoro.

Aidha amesema kuwa wote walioko katika maeneo hayo wanapaswa kutambua kwa sasa si wamiliki wa maeneo hayo hadi hapo uhalali utakapofanyika ambapo zoezi hilo la kupata uhalali litafanyika kupitia timu hiyo yenye vifaa vya kutosha kutoka wizarani na kuhusisha uongozi wa wilaya na wananchi ambapo baada ya uhakiki na mapendekezo utafanyika mchakato wa ugawaji wa mashamba hayo utakaofanyika chini ya Wizara ya Ardhi na kwamba kila anyemiliki mashamba hayo atambue kuwa kuanzia sasa si wamiliki hadi hapo uhakiki na ugawaji utakapofanyika upya.

Sambamba na hayo amewataka wananchi wa maeneo yote yaliyo na mashamba yaliyofutwa kutoa ushirikiano na kuachana na hulka ya kugomea uhakiki unapofanyika kwani kitendo cha kugomea timu hiyo kutapelekea kukosa haki yao ya umiliki na kwamba timu hiyo haitosita kuendelea na kazi iliyokusudiwa lengo ikiwa ni kutoa uhalali wa ardhi ili kila anayepaswa kumiliki aweze kumiliki kiuhalali na kuepusha migogoro ama kuitwa wavamizi.

Naye Mkuu wa Idara ya Ardhi na Maliasili Wilaya Ibrahim Ndembo ameushukuru uongozi wa Serikali ya awamu ya tano  kwa juhudi wanazofanya katika kufuta mashamba yasiyoendelezwa ambapo hadi sasa jumla ya mashamba pori 25 yenye ukubwa wa ekari 23,596 yamebatilishwa katika maeneo ya Msowero Mvumi na Chanzuru ambapo mashamba 15 kati ya 25 yakiwa yamebatilishwa katika kipindi cha uongozi wa awamu ya tano baada ya wamiliki wake kushindwa kuyaendeleza sambamba na mashamba pori 8 yenye ekari 3816 kwa maeneo ya Magole na Masanze taarifa zake zimewasilishwa kwa kamishna wa ardhi kwa ajili ya hatua za ubatilishwaji.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa