• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

UNDENI VIKUNI KUPATA FURSA MBALIMBALI- MKITI MKOPI

Posted on: October 26th, 2018

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilayani ya Kilosa Mhe. Hassan Mkopi ametoa rai kwa wanachama wa shirika lisilo la kiserikali – Campaign For Female Education(CAMFED) kujiunda katika vikundi na kujisajili ili kundi linalojulikana kisheria jambo litakalowasaidia kufaidika na fursa mbalimbali zinazojitokeza ikiwemo mikopo na mitaji kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi.

Mkopi amesema hayo Oktoba 26 mwaka huu wakati wa hafla fupi ya kukabidhi mitaji mbalimbali kwa wanachama hao walio chini ya CAMFED na kusema kuwa mitaji hiyo ikatumike kama ilivyokusudiwa kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi na kutumia vyema elimu waliyonayo ikiwemo kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha.

Aidha amesema kuwa mitaji hiyo inahitajika kukua na yeye kama Mwenyekiti kwa kushirikiana na madiwani wenzake watafanya ufatiliaji kuona namna wanavyojiendesha huku akisisitiza wanachama hao kutokuwa waoga kuwatumia wataalam mbalimbali katika kukuza mitaji yao ikiwemo benki ya NMB pamoja na wataalam toka idara ya maendeleo ya jamii pamoja na idara nyinginezo.

Akisoma risala ya wanachama wa CAMFED Katibu wa mtandao wa Camfed Members Association(CAMA) Kilosa na Kitaifa Bi. Mzizi Mtambua amesema shirika hilo lenye lengo la kuwasaidia watoto wa kike walio katika mazingira hatarishi ili waweze kujikwamua kielimu pia kuondokana na umaskini mpaka sasa linafadhili shule za sekondari 28 na shule za msingi 54.

Aidha amesema kuwa shirika hilo linajivunia wasichana 1226 waliowahi fadhiliwa na CAMFED ambao wanajihusisha na shughuli mbalimbali ikiwemo ujasiliamali, kilimo, kujitolea kufundisha stadi za maisha katika shule za sekondari n.k

Katika hafla hiyo ya ugawaji mitaji hiyo kwa wanacama 2000 vimekabidhiwa vifaa, vitendea kazi pamoja na bidhaa za kuuza vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 84 ili kuwanufaisha katika miradi mbalimbali ambayo itasimamiwa na wataalam wote wa Halmashauri kiujumla , kamati ya CAMFED Wilaya watendaji wa vijiji na kata pamoja na waratibu wa CAMFED ili kuongeza nguvu katika miradi watakayoifanya ili wafikie malengo waliojiwekea.

Sambamba na hayo Mwenyekiti wa halmashauri ameuagiza  uongozi wa Halmashauri kuandaa barua itakayoonyesha kuthamini mchango wa CAMFED kwani wamekuwa msaada mkubwa kwa kusomesha wanafunzi mbambali kwa gharama kubwa kazi ambayo ilipaswa ifanywe na Halmashauri.

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • ZABUNI January 31, 2017
  • SOMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA March 24, 2017
  • UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA March 24, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • Kilosa kufanya sensa ya mifugo

    December 29, 2022
  • Kilosa kunufaika na mradi wa BOOST

    December 24, 2022
  • Kilosa yaendelea kutambua juhudi za Serikali kwa Watumishi wa Umma na Wananchi-DED Kilosa

    December 19, 2022
  • -Serikali haitosita kulinda Rasilimali watu kwa maslahi ya Maendeleo ya Taifa- Mh. Mhagama

    December 20, 2022
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa