• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

UNGENI MKONO JITIHADA ZA SERIKALI KUPATA MAJI SALAMA - DC KILOSA

Posted on: October 30th, 2018

Rai imetolewa kwa wadau wote wilayani Kilosa kuunga mkono jitihada za serikali na Shirika la Misaada la Watu wa Marekani (USAID) pamoja na taasisi mbalimbali kuhakikisha upatikanaji wa maji safi, salama na yakutosha ili kutimiza azma ya Serikali ya awamu ya Tano ya Tanzania ya viwanda kwa kuchangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi pasipo kusahau usimamizi mzuri wa miradi ya maji.

Rai hiyo imetolewa Oktoba 30 mwaka huu na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe. S. Kebwe katika hafla ya uzinduzi wa miradi ya maji iliyotekelezwa na jamii kwa kushirikiana na mradi wa WARIDI katika kijiji cha Msowero kata ya Msowero wilayani Kilosa amesema kuwa mradi unalenga kuboresha upatikanaji wa maji kwa kuimarisha usimamizi endelevu wa rasilimali maji kwa manufaa ya kizazi hiki na kijacho pia unalenga dira ya maendeleo ya taifa ili kuimarisha usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji na kuhakikisha kuongezeka kwa idadi ya wananchi wanaopata maji safi na salama ifikapo 2025.

Mgoyi amesema kuwa maji ni muhimu katika maisha yetu kwani kumekuwa na matukio ya magonjwa ya kipindupindu hali ambayo imekuwa ikichangiwa kwa kukosa maji safi, salama na ya uhakika, hivyo mradi huo ni mkombozi hasa kwa kinamama kwa shughuli za kila siku ambazo kwa kiasi kikubwa zilikuwa zikiathiriwa na ukosefu wa maji, hivyo uwepo wa mradi huo utapunguza tatizo la ugonjwa wa kipindupindu na magonjwa mengine yatokanayo na ukosefu wa maji safi na salama ikiwemo kuwapunguzia mzigo mkubwa kinamama wa kutafuta maji.

Akisoma taarifa fupi ya mradi kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji Asajile Mwambambale Injinia Josh Chum amesema mradi huo ulikuja na sera ya kuwa na vyoo bora kwanza ambapo kwa hamasa ya wananchi waliweza kuchangia rasilimali fedha pamoja na nguvu kazi ambapo kiujumla mradi umegharimu shilingi milioni 469,237,660/= na kwa kupitia mradi wa WARIDI wananchi wamepunguza matatizo ya maji kwa 85%, kukuza uchumi kwa kutopoteza muda mwingi kutafuta maji safi, kuongeza kipato kwa kulima mbogamboga na ufugaji kuku kwa kutumia maji kidogo na kuongeza kipato cha kijiji kupitia mfuko wa maji kwa kuchangia huduma za maji.

Aidha Josh amesema kijiji cha Msowero kwa kushirikiana na mradi wa WARIDI, kampuni ya Water Pay na Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa wanakusudia kufunga mita za maji za kabla ya malipo katika vituo 26 vya kuchotea maji vya kijamii lengo ikiwa ni kuongeza ufanisi wa kutoa maji kwa jamii na kuongeza mapato ambapo ufungaji huo wa mita upo katika hatua za uhamasishaji na mafunzo kwa jumuia ya watumia maji kuhusu namna ya kutumia mfumo huo kabla ya kufungwa mita hizo.

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • ZABUNI January 31, 2017
  • SOMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA March 24, 2017
  • UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA March 24, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • Kilosa kufanya sensa ya mifugo

    December 29, 2022
  • Kilosa kunufaika na mradi wa BOOST

    December 24, 2022
  • Kilosa yaendelea kutambua juhudi za Serikali kwa Watumishi wa Umma na Wananchi-DED Kilosa

    December 19, 2022
  • -Serikali haitosita kulinda Rasilimali watu kwa maslahi ya Maendeleo ya Taifa- Mh. Mhagama

    December 20, 2022
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa