• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

UPATIKANAJI WA DAWA NI WA KURIDHISHA KILOSA - UMMY

Posted on: March 1st, 2019

Imeelezwa kuwa hali ya upatikanaji wa dawa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa imekuwa ya kuridhisha jambo linaloonyesha juhudi kubwa za kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais wa awamu ya Tano ikiwa ni sehemu ya ahadi zake kuwa atahahakikisha upatikanaji wa dawa unakuwa wa kuridhisha ikiwa ni ishara ya kuonyesha matokeo halisi ya fedha zinavyotumika.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Afya Dkt. Ummy Mwalimu ambapo amesema kwa kuwa upatikanaji wa dawa ni mzuri hivyo amewasisitiza madaktari kuhakikisha utoaji wa dawa kwa wagonjwa unazingatia mwongozo wa taifa wa matibabu ambapo amemtaka Mkurugenzi Mtendaji pamoja na Katibu Tawala Wilaya kuendelea kuwasisitiza madaktari kuzingatia mwongozo wa ugawaji dawa ka kadri unavyosema badala ya kugawa dawa kwa matakwa yao au ya  mgonjwa.

Akizungumzia upatikanaji wa dawa pamoja na upatikanaji wa huduma za matibabu mwalimu amewataka maafisa maendeleo ya jamii kuwahamasisha wananchi kukata bima ya afya iliyoboreshwa ili waweze kupata huduma stahiki ikiwemo kupata dawa bila ya kukutana na kikwazo cha kifedha na kwamba mwananchi aliye na bima ya afya atapata huduma zote bure katika zahanati,vituo vya afya na hospitali.

Aidha mwalimu amesisistiza kujengwa kwa jengo jipya la wagonjwa wa nje(OPD) kwani lililopo sasa ni chakavu na halina mazingira ya kuridhisha ya utoaji huduma na kwamba ameishauri ofisi ya mkurugenzi kupanga kuwa na hospitali nyingine lengo ikiwa ni kusogeza huduma kwa wananchi na kwamba kwa upande wa serikali itajenga miundombinu ya afya kulingana na mazingira hapa nchini na kusisitiza upatikanaji na utoaji wa chanjo mbalimbali kwa wananchi hasa watoto chini ya miaka mitano kwani mahitaji ya chanjo ni makubwa.

Sambamba na hayo amesisitiza kuzingatiwa kwa afya ya mama na mtoto kwa kupunguza idadi ya vifo vya watoto na vifo vitokanavyo na uzazi kwani teknolojia ipo pamoja na vifaa kwani wanawake wengi wanachelewa kuanza kliniki, hivyo ni vyema kinamama wanapojiona wana dalili za ujauzito kuanza kliniki mapema jambo litakalosaidia kupata huduma stahiki ili kulinda afya ya mama na mtoto ili wawe salama.

Licha ya kutoa maelekezo na mambo ya kuzingatia Mwalimu ametoa pongezi kiujumla kwa huduma za afya zinazotolewa katika hospitali ya Wilaya huku akisisitiza ujenzi wa vyoo bora kwa kaya ambao hazina vyoo bora na kuzingatia utoaji wa elimu ya kinga na kusisitiza lishe bora kwa wananchi.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa