• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO KWA KIPINDI CHA AWAMU YA SITA

Posted on: November 3rd, 2023

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Ndg. Kisena Mabuba ameishukuru Serikali ya Awamu ya 6 chini ya Uongozi wa Rais Dokta Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia Kilosa fedha kwaajili ya Utekelezaji wa Miradi mbalimbali ya Maendeleo katika Sekta ya Elimu, Afya, Kilimo na Mifugo, miundombinu pamoja na maji  na kusema kuwa fedha hizo zimeleta tija na kuchochea maendeleo kwa wana Kilosa.

Mkurugenzi huyo ametoa shukrani hizo kwa niaba ya wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa 02 Novemba 2023 wakati wa kikao na waandishi wa habari  katika kampeni ya kutangaza mafanikio ya Serikali ya awamu ya sita kilichofanyika  katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro  na kushirikisha wadau mbalimbali wa Habari na wakurugenzi 9 kutoka Mkoa wa Morogoro.

Mabuba amesema kuwa katika sekta ya afya kwa kipindi cha miaka mitatu halmashauri imepokea fedha kutoka serikali kuu kiasi cha shilingi 5,565,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya 5, Zahanati 18, ikiwemo Majengo ya X-ray , Wodi za mama na mtoto, nyumba za watumishi 3 pamoja na kiasi cha shilingi 1,350,000,000 kimepokelewa kwa ajili ya vifaa tiba vinavyotumika katika vituo vya kutolea huduma za afya  hivyo kurahisisha upatikanaji   wa huduma kwani  hapo awali wananchi walikuwa wanalazimika kutembea umbali mrefu kupata huduma hizo.

Sambamba na hayo amesema kuwa katika Sekta ya Elimu Halmashuri imepokea kiasi cha shilingi 2,046,000,000 kutoka serikali kuu kupitia mradi wa BOOST kwa ajili ya ujenzi wa shule 6 za awali na msingi pamoja na kiasi cha shilingi milioni 200,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu 4 , Katika Mradi wa SEQUIP halmashauri imepokea kiasi cha fedha shilingi  2,526,995,275 kwa ajili ya ujenzi wa Shule 5 za Sekondari ikiwemo  na kiasi cha shilingi 190,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu 4, Hivyo kurahisisha mazingira ya kusomea na kufundishia kwa wanafunzi.

 Aidha Mkurugenzi huyo amebainisha kuwa kwa sasa adha ya kutembea umbali mrefu ili kufika shuleni na Mrundikano wa Wanafunzi katika madarasa umepungua hali iliyochochea wananchi kujitokeza kwa wingi katika kuandikisha watoto kujiunga na Elimu ya awali na Msingi, huku utoro wa wanafunzi ukipungua kwa kiasi kikubwa

Mabuba ameongeza kwa kusema kwa kipindi cha miaka mitatu Vikundi mbalimbali vimepokea mkopo jumla ya kiasi cha shilingi bilioni 1,205,924,367.84 kwa ajili ya kufanya shughuli za kimaendeleo ili waweze kujikwamua kiuchumi, Mikopo ambayo inatokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri, na kusema kuwa vikundi hivyo ni kama vikundi vya wanawake 41, Vijana 31 na watu wenye ulemavu 31.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa