• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

UZINDUZI UJENZI VITUO VYA AFYA MALOLO NA MIKUMI WAFANA

Posted on: September 1st, 2018

Viongozi mbalimbali wa Halmashauri na Wilaya ya Kilosa wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi wameshiriki hatua ya awali ya ujenzi wa vituo vya afya Mikumi na Malolo kwa kushiriki kuchimba msingi wa vituo hivyo ambapo licha ya viongozi hao kushiriki Jeshi la Wananchi, wanafunzi wa Chuo cha Ufundi Mikumi VETA, Wakuu wa Idara , Makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na wananchi wameshiriki katika uzinduzi huo.

Akizindua ujenzi wa vituo vya afya kwa kata ya Mikumi na Malolo kwa njia shirikishi ya kuchimba msingi Mgoyi amesema kuwa viongozi hao wameshiriki katika ujenzi huo ikiwa ni njia ya kupungaza gharama za kuwalipa mafundi lakini pia kuunga mkono juhudi za Mhe. Rais John Magufuli katika kutekeleza ilani ya uchaguzi kwa kuhakikisha wananchi wanaondokana na adha ya upatikanaji wa huduma za afya  kwa kuhakikisha kila kata inakuwa na kituo cha afya.

Akielezea kuhusu kituo cha afya cha Mikumi Mgoyi amesema Mhe Rais wa awamu ya tano ametoa shilingi milioni 420 ili kuhakikisha kata hiyo inakuwa na kituo hicho ambacho kwa upande wa Halshauri watachangia kwa mujibu wa bajeti iliyopangwa pamoja na wananchi wakichangia nguvu kazi huku kwa upande wa kituo cha afya Malolo shirika la TAZAMA litachangia zaidi ya shilingi milioni 135 kwa ajili ya ujenzi huo .

Aidha katika uzinduzi wa ujenzi wa kituo cha afya Malolo Mkuu wa Wilaya huyo alifanya changizo ambapo Ofisi ya Mkuu wa Wilaya itachangia mifuko 200, Halmashauri katika bajeti yake ya 2019/20120 watatoa mifuko ya saruji 300, Mwenyekiti wa CCM Wilaya Ameir Mbarak ameahidi mifuko 100 ya saruji, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU wakiahidi mifuko 10 ya saruji, madiwani wa Tarafa ya Mikumi wakiahidi kuchangia mifuko 50, huku  wananchi wa kata ya Malolo wakitakiwa kuhakikisha wanachangia tofari laki moja kwa vitongoji vyote vya Malolo.

Naye Mkuu wa Idara ya Afya Dkt. Halima Mangiri amesema Kituo cha Afya Mikumi wanatarajia kujenga jengo la mapokezi, maabara, wodi ya kina mama na jengo la upasuaji huku Kituo cha Afya Malolo wakijenga jengo la wodi ya wazazi, maabara na jengo la mapokezi ambapo huduma mbalimbali zitapatikana katika vituo hivyo ikiwemo upasuaji kwa kinamama walioshindwa kujifungua kwa njia ya kawaida, matibabu kwa wagonjwa wa nje na  vipimo mbalilmbali ikiwemo upimaji wa damu, figo na ini.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa