• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

VIJANA 22 WILAYANI KILOSA WANUFAIKA NA MRADI WA SUMUKUVU

Posted on: August 14th, 2023

Vijana 22 kutoka maeneo mbalimbali Wilayani Kilosa wamekabidhiwa vifaa chuma vyenye thamani ya shilingi milioni moja na nusu kwa kila mmoja bure na Wizara ya kilimo kwa kushirikiana na VETA kupitia Mradi wa SUMUKUVU kwaajili ya kutengenezea vihenge vya kuhifadhia nafaka lengo likiwa ni kumsaidia  Mkulima kupata nyenzo sahihi ya kuhifadhia nafaka mara baada ya mavuno,na pia kujiajiri wao wenyewe

Hayo yameelezwa na Mhandisi Jeseph Kivako ambaye ni Afisa Ufuatiliaji na Tathmini ya mafunzo,  na pia Mratibu wa Sumukuvu VETA katika kikao cha kukabidhi vifaa hivyo  Agosti 11 ,2023 ambapo amesema kuwa VETA imeingia makubaliano na Wizara ya Kilimo kwa lengo la kushirikiana kufundisha vijana kuondoa athari za Sumukuvu kwenye mazao ya nafaka hususan Mahindi na Karanga.

Mhandisi Kivako amesema kuwa Sumukuvu inapatikana kabla na baada ya kuvuna huku kukiwa  vipengele viwili vikubwa ambavyo ni  uhifadhi na ukaushaji wa mazao ambapo amefafanua kuwa Mradi huo umejikita katika uhifadhi wa  nafaka hivyo  Wizara ya Kilimo kupitia mradi wa Tanpack pamoja na kujenga Maghala makubwa pia wameona  umuhimu wa wakulima wa kawaida kupata nyenzo sahihi ya kuhifadhia nafaka ambayo ni vihenge vya chuma.

Kivako amesema kwa kuzingatia hilo VETA imetoa mafunzo kwa vijana 420 kutoka Tanzania bara na visiwani na kuwatunukiwa Vyeti ambapo kati yao vijana 22 wametoka Wilayani Kilosa na kwamba mafunzo hayo yatawasaidia kutambulika,pia yatawawezesha  kuwasaidia wakulima kwa kuwaelimisha juu ya faida ya uhifadhi nafaka kapitia  Vehenge vya chuma,na ni matumaini yao kuwa kundi hilo litaenda kutengeneza fursa za ajira katika maeneo yao kupitia vifaa hivyo walivyopewa.

Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Kisena Mabuba amesema kuwa Teknolojia hiyo ya uhifadhi wa nafaka kwa kutumia Vihenge hivyo itatoa suluhu ya tatizo la Sumukuvu katika mazao,hivyo  amewataka vijana hao kufanya kazi kwa bidii na pia kutumia vifaa hivyo kwa malengo yaliyokusudiwa na pia waweze kutoa ujuzi huo kwa vijana wengine katika maeneo yao

 

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 KWA SHULE ZA SEKONDARI HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOSA July 14, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI September 16, 2023
  • ZABUNI January 31, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • KILOSA KUDUMISHA USAFI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    September 20, 2023
  • TIMU YA UKAGUZI MKOA YATEMBELEA MIRADI YA BOOST KILOSA

    September 20, 2023
  • MAPATO YA HALMASHAURI YAONGEZEKA KUTOKA ASILIMIA 94 MPAKA ASILIMIA 98.91

    September 01, 2023
  • Walimu watakiwa kuendelea kuzifahamu huduma za kibenki

    August 29, 2023
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa