• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

DC KILOSA APIGA MARUFUKU MICHANGO HOLELA ISIYO NA KIBALI

Posted on: October 20th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mh. Majid Mwanga amewataka viongozi katika Kata na vijiji kuhakikisha michango yote inayochangishwa katika maeneo yao inakuwa na kibali kutoka kwa Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji kwani kumekuwa na hulka ya baadhi ya viongozi kuchangisha michango kiholela bila kufuata taratibu za upatikanaji wa kibali.

Mwanga ametoa rai hiyo wakati alipozungumza na wananchi wa kijiji cha Kitunduweta katika kata ya Mhenda ambapo amesema kuwa kumekuwa na baadhi ya viongozi wamekuwa wakikiuka taratibu za uchangishaji michango jambo ambalo si sahihi huku akitaka michango iliyokuwa inaendelea kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari katika kata ya Mhenda kusimama mara moja kwani tayari Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ameshatoa shilingi milioni 600 kwa ajili ya shule ya sekondari, hivyo hakuna haja ya mchango huo kuendelea ambapo amesisitiza kuwa hakuna michango inayozuiwa endapo itafuata taratibu za kupata kibali.

Aidha amekipongeza Kijiji cha Kitunduweta kwa namna kilivyoweza kuhifadhi vyema msitu wa kijiji uliopo katika hali ya uendelevu licha ya shughuli za uvunaji mkaa kuendelea lakini kupitia elimu na uwezeshwaji kutoka MJUMITA na TFCG msitu huo umekuwa katika hali ya uendelevu huku akitoa rai kwa TFCG kutafuta fedha kwa lengo la kufanya oparesheni maalum ya  kurejesha msitu wa Ukwiva ili urejee katika hali yake ya zamani.

Akizungumzia suala la ulimaji bangi amesema wapo baadhi ya viongozi na wananchi wamekuwa wakishiriki katika kilimo cha bangi ambacho hivi karibuni Kamati ya Ulinzi na Usalama ilifanya oparesheni maalum katika misitu wa Ukwiva ambao umeharibiwa sana hususanivyamvyo vya maji ambavyo vimeharibiwa kwa kiasi kikubwa huku shughuli za kibinadamu zikiendelea ikiwemo kilimo cha bangi.

 Mwanga amesema katika operesheni hiyo kamati ya ulinzi na usalama ilifanikiwa kuteketeza zaidi ya heka kumi za zao la bangi ambapo tayari wahusika wameshakamatwa na kuchukuliwa hatua huku akisema kuwa lengo la operasheni hiyo kupambana na madawa ya kulevya ya aina mbali ni sehemu ya kutekeleza agizo la Mheshimiwa Rais katika kupambana na madawa ya kulevya na kwamba kilimo hicho katika Wilaya ya Kilosa hakikubaliki hata kidogo kwani ulimaji bangi umekua ukichangia kwa kiasi kikubwa kuharibu vijana ambao ni taifa la kesho.

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • ZABUNI January 31, 2017
  • SOMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA March 24, 2017
  • UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA March 24, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • Kilosa kufanya sensa ya mifugo

    December 29, 2022
  • Kilosa kunufaika na mradi wa BOOST

    December 24, 2022
  • Kilosa yaendelea kutambua juhudi za Serikali kwa Watumishi wa Umma na Wananchi-DED Kilosa

    December 19, 2022
  • -Serikali haitosita kulinda Rasilimali watu kwa maslahi ya Maendeleo ya Taifa- Mh. Mhagama

    December 20, 2022
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa