• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

VIONGOZI HAKIKISHENI TARATIBU ZA UDHIBITI CORONA ZINAFUATWA KATIKA MAENEO YENU

Posted on: April 21st, 2020

Wakati janga la ugonjwa wa corona likiendelea katika maeneo mbalimbali hapa nchini Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi ameitaka jamii kufahamu kuwa ugonjwa wa corona ni ugonjwa hatari hivyo amewataka viongozi wa dini, tarafa, kata na vijiji kuendelea kuzingatia taratibu za kudhibiti zinazoelekezwa na wataalam wa afya kwa kuhakikisha taratibu hizo zinasimamiwa ipasavyo katika maeneo wanayoyasimamia lengo ikiwa ni kuzuia maambukizi ya virusi vya corona.

Mgoyi amesema hayo wakati wa kikao chake na viongozi mbalimbli wa dini, maafisa tarafa na watendaji wa kata ambapo ametaka kila mmoja kuwajibika kwa sehemu yake kwa kuhakikisha taratibu zote zilizoelekezwa zinafanyika na kufuatwa ambapo amesema sheria za mbalimbali ikiwemo za afya, sheria ndogo, sheria za usafi na nyinginezo zinafuatwa hususani taratibu za kufuata ili kudhibiti maambuklizi ya virusi vya corona kama zinazovyoelekezwa na wataalam wa afya pamoja na kuzingatia unawaji mikono kwa maji tiririka na sabuni,  katika kudhibiti virusi vya corona zinazopaswa kufutwa, ukaaji wa umbali wa mita moja toka mtu mmoja kwenda mtu mwingine na sheria nyinginezo.

Pamoja na hayo Mgoyi amesema ipo haja ya kuendelea kukumbushana na kuhakikisha kila mmoja anawajibika kwa sehemu yake ndani ya jamii anayoingoza na kwamba wilaya ya Kilosa ina njia nyingi za watu kuingia katika wilaya hivyo ni vema umakini ukaongezeka katika kudhibiti maambukizi ya virusi vya corona kwani ugonjwa huu ni hatari na kwamba shughuli zote katika jamii hazizuiwi isipokuwa kila mmoja anapaswa kuzingatia sheria na taratibu huku akiwataka viongozi hao kuzingatia na kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwa jamii wanayoingoza huku akisema kuwa kwa yoyote ambaye hatazingatia sheria hizo eneo lake litafungiwa.

Aidha amewataka watendaji wa kata na maafisa tarafa kuhakikisha wanafanya wajibu wao ipasavyo na kwamba mtendaji yoyote ambaye hatawajibika katika nafasi yake hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yake huku akitoa wito kwa wadau na wafanya biashara mbalimbali kuungana na wilaya kwa ujumla katika kuchangia mahitaji mbalimbali ya vifaa kwa ajili ya kudhibiti maambukizi ya virusi vya corona ambapo pia amewataka wamiliki wa vituo vya afya na zahanati binafsi kuunga mkono juhudi za wilaya katika kudhibit virusi vya corona kwa kutoa michango yao ambapo pia amesema kwa vyombo vyote vinavyosafirisha abiria ikiwemo noah na mabasi kutakuwa na utaratibu wa upuliziaji dawa katika vyombo hivyo kila vyombo hivyo vinapoingia wilayani.

Naye Katibu Tawala Wilaya Kilosa Yohana Kasitila amesema viongozi wa dini wanayo nafasi kubwa ya kuingoza jamii kwa kumuomba Mwenyezi Mungu ili atunusuru katika janga la corona na kwamba viongozi  hao wanao wajibu wa kushirikiana na wilaya katika kuwasaidia wananchi walio chini yao kwa kuhakikisha wanashiriki katika nyumba za ibada kwa kukaa katika umbali unaotakiwa, kunawa mikono kwa maji safi tiririka na sabuni ili waweze kumwabudu Mungu wakiwa salama ambapo upande wa watendaji wa kata na maafisa tarafa wametakiwa kusimamia maeneo yao kwa kuendelea kuhamasisha jamii kuendelea kujikinga na maambukizi ya virusi vya corona.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa