• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

VIONGOZI WA DINI, TARAFA NA KATA WAASWA KUHAKIKISHA MAENEO WANAYOONGOZA YANAZINGATIA MAELEKEZO DHIDI YA VIRUSI VYA CORONA

Posted on: April 22nd, 2020

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale ametoa wito kwa viongozi wa ngazi mbalimbali wa kiserikali na kidini walioko wilayani Kilosa kuungana kwa pamoja kuendelea kujenga msingi imara juu ya uelewa wa udhibiti wa maambukizi ya virusi vya covid 19 lengo ikiwa ni kuhakikisha wilaya inakuwa salama kwani mpaka sasa baadhi ya wananchi wameendelea kuchukua hatua za awali wa kuweka ndoo na sabuni katika maeneo yao licha ya kwamba kuna baadhi ya wananchi hawako tayari kunawa mikono ikiwa ni sehemu mojawapo ya kujikinga na virusi vya corona.

Mwambambale amesema kuwa yapo baadhi ya maeneo watu wameweka ndoo za maji lakini zikiwa hazina maji na maeneo mengine ndoo zina maji lakini watu wamekuwa hawataki kunawa na kwamba kunawa kwa kipindi hiki cha maambukizi ya corona ni suala la lazima hivyo amewataka viongozi hao kuendelea kusimamia maagizo yanayotolewa na viongozi wa ngazi za juu na kwamba hadi sasa ugonjwa wa corona upo katika maambukizi ya ngazi ya kijamii hivyo ni vema watu wakaendelea kuchukua tahadhari kwa kuzingatia maelekezo ya viongozi na wataalam wa afya wanavyoelekeza.

Aidha amesisitiza viongozi hao kuhakikisha michezo mbalimbali inayokusanya watu wengi kwa wakati ambayo ni vigumu kuzingatia taratibu za udhibiti wa kusambaa kwa virusi vya covid 19 kama vile uchezaji wa mpira wa miguu unaondelea katika maeneo mbalimbali ameelekeza kusitishwa kwa mechi hizo sambamba na mazoezi mbalimbali yanayohusisha mkusanyiko, huku akisisitiza kusimamishwa kwa vibanda mbalimbali vinavyoonyesha picha mbalimbali za video almaarufu kama vibanda umiza ambavyo kwa asilimia kubwa vinahusisha mikusanyiko ya watoto na watu wazima pamoja na kutohusishwa kwa watoto katika kutembeza biashara mbalimbali mitaani.

Akibainisha maagizo muhimu ya kutekeleza katika tarafa, kata, vijiji na nyumba za ibada ili  kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa virusi vya corona Mkuu wa Idara ya Afya Kilosa Dkt. George Kasibante amesema maafisa tarafa, watendaji wa kata na vijiji wanao wajibu wa kuhuisha na kusimamia Kamati za Afya za kata na vijiji, Kusimamia maeneo yao kwa kuhahakisha kanuni zote za kujikinga na ugonjwa wa homa kali ya mapafu (COVID-19) zinafuatwa, Kuzuia mikusanyiko kwenye pull table, mashine za bahati nasibu(slots machines), mabanda ya video, vilabu vya pombe, baa, minada, harusi, misiba na maeneo ya kutolea huduma mbalimbali, Kuhakikisha baa na vilabu vya pombe wanafungua baada  ya muda wa kazi, kuhakikisha kunakuwepo na ndoo za maji tiririka na sabuni za kunawia mikono kwenye maeneo ya biashara na nyumba za kuishi.

Pia kuhakikisha wananchi wa maeneo yao wanapunguza safari zisizo za lazima, Kuwafatilia na Kuwatambua wageni wanaoingia na kuwaripoti kwenye mamlaka husika wanapokua na wasiwasi na afya zao, Kutoa ripoti kila siku ya elimu ya afya kwenye maeneo yao, Kufanya ukaguzi na utekelezaji wa hatua za kujikinga na maambukizi ya Corona hasa maeneo ya mikusanyiko, Kuwachukulia hatua wale wote ambao hawataki kufuata taratibu zilizotolewa, Kutoa elimu kwa viongozi na wananchi kuhusu namna ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona (COVID-19). – WDC, Halmashauri, Kuzuia michezo inayokusanya watu wengi kwa wakati mmoja na ambayo ni vigumu kuzingatia taratibu za kudhibiti na kuingiza ajenda ya COVID-19 katika vikao vyao kwenye ngazi mbalimbali.

Kwa upande wa viongozi wa dini Dkt. Kasibante amesema wanao wajibu wa kuhakikisha kunakuwa na ndoo za maji tiririka na sabuni kwenye nyumba za ibada wanazoziongoza, Kuweka mtu maalumu atakayesimamia uwepo wa maji na sabuni na kuhakikisha watu wote wanaongia na kutoka kwenye nyumba za ibada wana nawa mikono yao, Kuhakikisha watu wanakuwa mbalimbali (mita 1) wakati wa maandalizi ya ibada na wakati wa kufanya ibada, Kufupisha muda wa kufanya ibada kwa baadhi ya madhehebu, Kuingia kwa awamu ya watu wachache kufanya ibada kwa baadhi ya madhehebu ili kupunguza mkusanyiko au msongamano, Kupulizia dawa kwenye nyumba za ibada baada ya ibada kuisha na kupokea mapendekezo ya viongozi wa dini juu kujikinga na ugonjwa wa COVID.

 

 

 

 

 

 

 

 

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa