• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

VIONGOZI WA DINI WATAKIWA KUSHIRIKI UTATUZI WA CHANGAMOTO

Posted on: June 28th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Alhaji Majid Mwanga ametoa rai kwa viongozi wa dini kuendlea kuhubiri amani katika nyumba za ibada huku wakiendelea kuvumiliana wakati uongozi ukiendelea kufanyia kazi changamoto mbalimbali zilizopo ndani ya wilaya.

Mwanga ametoa rai hiyo alipokuwa akizungumza na viongozi wa madhehebu ya dini zote Kilosa ambapo amesema ili kukabiliana na changamoto ni wajibu wa kila kiongozi kutafuta majawabu ya changamoto hizo kwa kuwa na uongozi wa pamoja huku akisema endapo zitapatiwa majawabu hakutakuwa na mabango, huku akisisitiza viongozi hao kuzungumzia mazuri na vivutio vilivyopo ndani ya wilaya ili kuvutia wawekezaji jambo litakalosaidia upatikanaji wa ajira kwa vijana waliopo Kilosa.

Akizungumzia suala la ulinzi amesema ulinzi uko katika maeneo mbalimbali ambapo kwa upande wake amesema kila mmoja analo jukumu la kumlinda mtoto wa kike ambaye kwa asilimia kubwa anakumbana na changamoto mbalimbali ambazo zinaweza kupelekea kutofikia ndoto zake, hivyo anapaswa kuwezeshwa kujitambua, kujiamini na kujithamini, huku upande wa vijana akisisitiza walindwe dhidi ya madawa ya kulevya pamoja na kukemea utoro mashuleni.

Kwa upande wa mashamba yaliyofutwa amesema upo utaratibu unaoendelea kufanyika hivyo wasiwe na wasiwasi kwani baada ya taratibu stahiki kukamilika mchakato wa ugawaji utakuwa wa wazi bila kificho huku akiahidi kufanya ziara za kutembelea vijiji vyote na kukutana na viongoz ili kuweka mkakati na kujenga uelewa wa pamoja lengo ikiwa ni kufanya kazi kwa pamoja kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu huku wakimtanguliza Mwenyezi Mungu.

Miongoni mwa changamoto zilizobainishwa na viongozi hao wa dini ni migogoro ya wakulima na wafugaji jambo linalopelekea hali ya uzalishaji na kipato kushuka, kukosa uendelevu wa maeneo muhimu, kutokarabatiwa tuta la mto Mkondoa, uhaba wa mashamba, kutopatikana kwa zaka ya kutosha katika nyumba za ibada kutokana na waumini kushinda mashambani kwa kuhofia kulishiwa mashamba yao na wafugaji wakiwa nyumba za ibada, wakulima kupigwa na wafugaji pamoja na migogoro ya ardhi.

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • ZABUNI January 31, 2017
  • SOMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA March 24, 2017
  • UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA March 24, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • Mfumo wa TAUSI watambulishwa kwa wafanyabiashara

    March 23, 2023
  • Shule ya Msingi Tambukareli yaanza kutumika rasmii

    March 06, 2023
  • Shule ya Msingi Tambykareli yaanza kutumika rasmi

    March 06, 2023
  • DC SHAKA ASISITIZA UONGOZI WA PAMOJA

    March 01, 2023
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa