• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

VIONGOZI WA TARAFA, KATA NA VIJIJI WAKUMBUSHWA KUWEKA MIKAKATI YA KUEPUKA MIGOGORO MSIMU WA KIANGAZI- DC

Posted on: September 12th, 2020

Viongozi wa tarafa, kata na vijiji wametakiwa kutimiza majukumu yao kwa kufanya kazi zao ikiwemo kusimamia maeneo yao na kuhakikisha amani inakuwepo hususani katika kukabiliana na migogoro katika kipindi cha kiangazi na msimu wa maandalizi ya mashamba.

Rai hiyo imetolewa Septemba 11 mwaka huu na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi wakati wa kikao chake na viongozi wa tarafa za Masanze, Ulaya, Kilosa mjini na Kimamba ambapo amewataka viongozi hao kutokuwa chanzo cha migogoro katika maeneo yao kwa kuhakikisha vikao vya amani na vya kisheria vinafanyika sambamba na kutopokea mifugo kiholela jambo linalosababisha mifugo kuongezeka kwa wingi.

Mgoyi amesema viongozi hao wanao wajibu wa kusimamia na kuhakikisha migogoro inaisha na kwamba suala hilo linahitaji uwajibikaji na yeyote ambaye ataonesha kutowajika ipasavyo hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yake huku akiwataka kuhakikisha wanahakiki idadi ya mifugo jambo litakalosaidia kutambua mifugo vamizi katika maeneo yao.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale ametoa onyo kwa viongozi hao kuacha mara moja hulka ya kukaribisha wageni kwa makubaliano yasiyo rasmi jambo ambalo limekuwa likisababisha migogoro huku akiwataka kufanya kazi kama timu na kuendesha shughuli zao kwa kufuata taratibu kanuni na sheria jambo litakalowasaidia kufanya kazi katika njia sahihi kwani serikali za vijiji ni mamlaka ambazo zinaweza kupokea changamoto na kuzimaliza kwa mujibu wa taratibu ikiwemo umalizaji kwa njia ya vikao.

Aidha Katibu Tawala Wilaya Yohana Kasitila amewataka viongozi hao kusimamia na kutekeleza maazimio yote yaliyotokana na kikao hicho ikiwemo utekelezaji wa agizo lililotolewa na Mkuu wa Wilaya ndani ya siku saba takwimu za idadi ya mifugo ziwe zimepatikana kwa kila eneo lakini pia kufanyika kwa tathmini za ukweli, sambamba na wenyeviti wa vijiji kutimiza wajibu wao, kukaa vikao vya kisheria, kutatua migogoro kwa kutafuta chanzo cha tatizo pamoja na kuepuka vitendo vya rushwa.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa