• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

VIONGOZI WAKUMBUSHWA KUZINGATIA MAADILI

Posted on: June 5th, 2023

Viongozi mbalimbali wilayani Kilosa wametakiwa kuzingatia zaidi maadili katika utendaji wa kazi za kila siku kwa kuhakikisha wanazingatia sheria, kanuni na taratibu za majukumu yao ya kila siku katika kuwatumikia wananchi.

Rai hiyo imetolewa Juni 5, 2023 na Afisa Maadili Kanda ya Mashariki Bw. Selemani S. Selemani wakati akizungumza na baadhi ya waheshimiwa madiwani pamoja na wakuu wa idara na vitengo ikiwa ni sehemu ya kukumbushana suala zima la maadili na uwajibikaji katika sekta ya Umma ambapo amesema viongozi wanapozingatia maadili inapelekea kuwepo kwa amani na uadilifu.

Selemani amesema kuwa katika kuhakikisha uwajibikaji unachukua nafasi yake ipo misingi ya uwajibikaji ambayo inapaswa kusimamiwa na kila mmoja ikiwemo kufanya maamuzi kwa kuzingatia sera, sheria, kanuni na taratibu, kupokea maoni na ushauri kama fursa ya kuboresha utendaji kazi, kufanya tathmini na kuendelea kujifunza kutokana na uzoefu, kupitia upya mifumo ya taasisi na kufanya maboresho ili kuendana na mabadiliko ya mazingira na kuongeza ufanisi na ubora, kuwa na kiu ya kufanya mambo katika ubora na endelevu pamoja na kujenga tabia ya ushirikiano.

Akibainisha aina za uwajibikaji amesema zipo aina kadhaa za uwajibikaji ikiwemo uwajibikaji binafsi, uwajibikaji wa kitaaluma, uwajibikaji wa kifedha, uwajibikaji wa kimaadili, uwajibikaji wa kiutawala na wa kampuni, huku akisema upo umuhimu wa wa uwajibikaji ikiwemo uwepo wa matumizi bora ya rasilimali za umma ili kufikia malengo ya Taifa, kudumisha uwazi katika utekelezaji na taratibu za kutoa maamuzi, kuhakikisha sheria, kanuni na taratibu zinafuatwa, kudhibiti matumizi mabaya ya madaraka, kutenda haki pamoja na kuimarisha imani ya wananchi kwa viongozi na Serikali yao.

Sambamba na hayo amesema katika kusimamia uwajibikaji zipo changamoto mbalimbali ikiwemo kutokuwa na imani na watumishi, kufanya kazi kwa mazoea, hofu ya kushindwa, ukosefu wa mawasiliano na ushirikiano kati ya kiongozi na watumishi pamoja na kutopenda ama kukosa muda wa kuendeleza watumishi.

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 KWA SHULE ZA SEKONDARI HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOSA July 14, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI September 16, 2023
  • ZABUNI January 31, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • KILOSA KUDUMISHA USAFI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    September 20, 2023
  • TIMU YA UKAGUZI MKOA YATEMBELEA MIRADI YA BOOST KILOSA

    September 20, 2023
  • MAPATO YA HALMASHAURI YAONGEZEKA KUTOKA ASILIMIA 94 MPAKA ASILIMIA 98.91

    September 01, 2023
  • Walimu watakiwa kuendelea kuzifahamu huduma za kibenki

    August 29, 2023
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa