• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WAAJIRIWA WAPYA WILAYANI KILOSA WANUFAIKA NA MAFUNZO ELEKEZI

Posted on: January 7th, 2025

 

Waajiriwa wapya wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa wamepatiwa mafunzo elekezi yaliyolenga kuwaandaa katika majukumu yao mapya.

Mafunzo hayo yametolewa 06 Januari, 2025 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ambapo mafunzo hayo yamehusisha mada muhimu zinazohusu maadili ya kazi, uwajibikaji, kufuata sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma.

Akizungumza katika kikao hicho Afisa Utumishi Ndg George Lazaro aliwataka waajiriwa wapya kutumia mafunzo hayo kama msingi wa utendaji bora na nidhamu kazini. Aliwasisitiza kuwa wanapaswa kujitahidi kuwa waadilifu, wabunifu, na kushirikiana na wenzao kazini ili kuimarisha huduma bora  kwa wananchi.

"Ninyi ni kundi jipya la watumishi mnaoingia kwenye mfumo wa halmashauri tunategemea mchango wenu mkubwa katika kuboresha huduma na maendeleo ya jamii yetu. Tunataka kuona nidhamu, uwajibikaji, na juhudi za dhati katika kila mnachofanya," alisema Lazaro.

Kwa upande wake Afisa Utumishi Ndg.Hussein Ayoub, aliwaeleza waajiriwa kuhusu haki na wajibu wao kama watumishi wa umma, akiwakumbusha kuwa utumishi wa umma ni dhamana kubwa inayohitaji uadilifu na weledi. Alieleza kuwa kwa kufuata maadili ya kazi na taratibu zilizowekwa wataweza kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kusaidia kufanikisha malengo ya halmashauri. "Tunawapa nyenzo za msingi za utumishi mnapaswa kuzingatia miongozo hii ili kufanikisha kazi zenu kwa weledi," alisema Ayoub.

Katika mafunzo hayo waajiriwa wapya walipata nafasi ya kuuliza maswali na kushiriki mijadala kuhusu changamoto mbalimbali wanazotarajia kukutana nazo. Mafunzo hayo yaliibua mijadala yenye tija kuhusu namna bora ya kushirikiana kazini na kutoa huduma bora kwa wananchi. Mafunzo hayo pia yalilenga kuwaelekeza waajiriwa kuhusu umuhimu wa kuzingatia sheria za utumishi wa umma na taratibu za kiutawala.

Naye Yamola Elias Daga mmoja wa waajiriwa wapya, alitoa shukrani kwa uongozi wa halmashauri kwa kuwaandalia mafunzo hayo muhimu. Alisema kuwa mafunzo hayo yatawasaidia kuelewa vyema majukumu yao mapya na yatawajengea uwezo katika majuku yao ya kila siku. "Tunaishukuru sana halmashauri kwa mafunzo haya tumepata maarifa mengi ambayo yatatusaidia kufanya kazi kwa weledi na ufanisi," alisema Yamola.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa