• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Wadau wa Kilimo, Mifugo, Utalii na Mazingira watakiwa kushiriki utatuzi wa changamoto za kilimo

Posted on: September 28th, 2022

Ili wananchi walime kwa tija tunahitaji kufanya mabadiliko ya kifikira , namna ya utendaji na mfumo kwani mkoa wa Morogoro ni mkoa wa pili kwa ukubwa nchini Tanzania  ukiwa na ongezeko kubwa la watu na eneo kubwa, lakini pia ni mkoa wenye migogoro mingi ya ardhi kutokana na watendaji kushindwa kusimamia wananchi vizuri katika matumizi ya ardhi ipasavyo.



Hayo yamebainishwa Septemba 28 mwaka huu na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mh. Fatma Mwassa wakati wa ufunguzi wa kongamano la wadau wa Kilimo likiwa na lengo la kuongeza hamasa kwa vijana kutambua kuwa Kilimo ni fursa katika kujipatia kipato na kujiajiri kwa kauli mbiu  inayosema “TUNAANZIA SHAMBANI”.


 ‘‘Licha ya ukubwa mkoa wa Morogoro wenye ardhi yenye rutuba mkoa umekuwa haufanyi vizuri katika uzalishaji mfano zao la mpunga unazalishwa kwa wastani wa tani 2.3 kwa ekari badala tani 6, mahindi tani 1.5 kwa ekari badala ya 6, viazi ni tani 2.6 badala ya tani 20 na ndizi tani 4.4 badala ya tani 35 na miongoni mwa sababu za uzalishaji usio na tija ni kilimo cha kutegemea mvua, matumizi ya mbegu za kienyeji, kutotumia mbolea au mbolea isiyo sahihi, kutokujua hali ya udongo na mazao inayostawisha pamoja na tabia ya watu kutenga eneo kubwa bila kujali uwezo wa kulihudumia ambapo kutokana na changamoto ya mvua na uzalishaji usio na tija mkoa umeamua kuchukua hatua za makusudi kuwa na kongamano ambalo litatupa fursa ya kujifunza, kutathmini na kuamua kwa pamoja nini kifanyike’’. Amesema Fatma Mwassa.


Wadau walioshiriki katika kongamano ni  wabunge, wahadhiri wa Vyuo Vikuu, wakulima, wauza zana za Kilimo na pembejeo na taasisi za Serikali kama TFS, NEMC, TAWA, TANAPA, na nyingine lengo ikiwa kujadili kwa pamoja namna ya kuondoa changamoto za kilimo zinazotokana na mwingiliano wa shughuli zinazofanyika na wadau husika.

Aidha uwepo wa kongamano hilo utaambatana na tukio la uzinduzi wa  msimu wa Kilimo 2022/2023 kimkoa unaotarajiwa kufanyika Oktoba 3 mwaka huu katika Wilaya ya Kilosa ambapo jumla ya Ekari 5496 zitagawiwa kwa wakulima ikiwa ni sehemu ya ardhi inayotokana na mashamba tisa (9) ambayo umiliki wake ulibatilishwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kuona mashamba hayo hayaendelezwi ambapo mashamba yanategemewa kupunguza uwepo wa migogoro ya ardhi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kongamano hilo Mh. Prof. Palamagamba Kabudi amesema uwepo wa kongamano hilo ni fursa nzuri ya utekelezaji wa shughuli za kilimo kwani mkoa wa Morogoro ni mkoa wa kipekee kwa shughuli za kilimo kutokana na ardhi iliyopo huku akimshukuru Mheshimiwa Rais kwa msukumo mkubwa aliouweka katika kilimo ikiwemo kuwezesha ujenzi tarajiwa wa skimu mbili kubwa katika mkoa wa  Morogoro ambapo moja inatarajiwa kuwepo katika wilaya ya Kilosa katika kata ya Rudewa.

Pro. Kabudi amesema uwepo wa kongamano hilo  litatoa mwelekeo wa namna ya kuendesha sekta ya kilimo ili kusukuma mbele maendeleo ya taifa kwani mkoa wa Morogoro una neema ya kuwa na ardhi nzuri inayofaa kwa kilimo na kwamba anaamini kupitia dhana ya siasa ni kilimo, kilimo kinapaswa kuwezesha upatikanaji wa mahitaji ya chakula kwa ajili ya wakulima na wasiolima, upatikanaji wa mazao ya kuuza nje na kuzalisha kwa ajili viwanda na kwamba kupitia kongamano hilo yatapatikana maazimio ambayo yanapaswa kutekelezwa.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa