• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WAFANYABIASHARA WAASA KUBUNI MIFUKO MBADALA

Posted on: June 3rd, 2019

Juni 3 mwaka huu Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi ametoa wito kwa wafanyabiashara kuwa wabunifu kwa kutengeneza mifuko mbadala ili kuepuka kupoteza wateja kutokana na uhaba wa mifuko uliopo sasa baada ya kuwepo katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo imebainika kuwa na athari kimazingira na kwa mifugo.

Mgoyi ametoa wito huo wakati wa zoezi la ukaguzi wa utekelezaji wa kuondoa mifuko ya plastiki madukani ambapo amewataka wafanyabiashara kuwa wabunifu ikiwemo kutengeneza mifuko kwa kutumia magazeti ili kutopoteza wateja kutokana na kukosa mifuko ya kuhifadhia bidhaa pia amewashukuru wafanyabishara kuitika zoezi hilo huku akitoa mwaliko kwa wafanyabiashara wakubwa kutengeneza mifuko na kuisambaza kwani ipo changamoto kubwa ya upatikanaji wa mifuko mbadala.

Kwa upande wa wafanyabiashara Mary Lyanzile na Hassan Kombo almaarufu mpemba wamesema pamoja na kuitika zoezi hilo wanakumbana na changamoto kubwa ya uhaba wa mifuko ambayo hupelekea kukosa wateja na kusababisha mapato yao kushuka lakini pia wamesisitiza kuongezwa kwa kiwango cha ubora wa mifuko kwani iliyopo kwa sasa inaonekana kukosa ubora, sambamba na hayo wametoa wito kwa wateja wao kutumia mifuko ya visalfeti inayoonekana kuwa imara pia wamepongeza usafi wa mazingira ambao umeanza kuonekana kwa baadhi ya maeneo ambapo mifuko ilikuwa ikizagaa.

Naye Janelove Thobias mfanyabiashara wa soko la Sabasaba amesema ni vema kwa mazingira yaliyopo sasa wafanyabiashara hasa wa sokoni wakajiongeza na kutengeneza mifuko nafuu ambayo ni gharama rahisi ili kutopeteza wateja kwani mifuko hiyo ni rahisi kutengeneza na haichukui muda mrefu kuitengeneza kwakuwa unatengeneza kwa kutumia gundi na magazeti ama makaratasi yaliyotumika.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kilosa Nathan Kaunda amesema kuwa zoezi hilo ni endelevu kwani kila siku takwimu za uwasilishaji mifuko zimekuwa zikiendelea kukusanywa kutoka katika kata zote na kwamba mifuko yote inayowasilishwa inakusanywa kwa ajili ya hatua nyingine zaidi ambapo Afisa Mazingira na Udhibiti takangumu Aloyce Simeono amesema hadi sasa mifuko 11,000/ imekwisha kukusanywa kutoka katika maeneo mbalimbali ambayo imesalimishwa katika kata mbalimbali.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa