• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WAHANDISI WA HALMASHAURI WAMETAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUEPUKA VITENDO VYA RUSHWA

Posted on: December 11th, 2023

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mussa Ali Musa amewataka Wahandisi wa majengo kufanya kazi Kwa weredi ili kuikamilisha miradi Kwa wakati uliopangwa huku akiwataka kujiepusha na vitendo vya rushwa.

Ameyasema hayo katika kikao cha pamoja cha majumuisho ya miradi ya ujenzi kilichofanyika katika Halmashauri ya Kilosa Disemba 7, 2023 na kujumuisha Halmashauri zote za mkoa wa Morogoro lengo likiwa ni kujenga uelewa wa pamoja na pia kujifunza teknolojia mpya zinazojitokeza kwenye sekta ya ujenzi.

Ameongeza kuwa baadhi ya Wahandisi hawafiki kuikagua miradi mara kwa mara huku wengine hawatoi ushirikiano wa kutosha kwa wale wanaosimamia na wanaotekeleza miradi hiyo wakiwemo mafundi na kuwataka waandae mipango kazi Ili kurahisisha kazi zao.

Aidha amewashauri Wahandisi kuhakikisha wanajenga hifadhi za maji katika miradi mipya husasani kwenye shule hasa za bweni Ili zirahisishe uzimaji wa moto endapo likitokea Janga la moto kwenye majengo hayo.

Katika kuzijibu changamoto wanazokumbana nazo Wahandisi hao katika kutekeleza majukumu yao, amezitaka mamlaka za kiutawala kuwapa ushirikiano Wahandisi hao huku akiwataka Wahandisi kuwa wabunifu katika kazi zao.

Kwa upande wake Mhandisi Mkuu wa Mkoa Mhandisi Ezron Kilamhama ambaye ndiye muandaaji wa kikao hicho, amesema kuwa lengo la kikao hicho ni kutambua hatua zilizofikiwa katika miradi mbalimbali kwa Halmashauri zote za mkoa lakini pia kubadilishana uzoefu baina ya Wahandisi wote na kuongeza kuwa utaratibu huu hufanyika Kila mwaka ambapo huchaguliwa Halmashauri mojawapo ya kufanyai kikao h icho.

Wakiwasilisha taarifa zao za miradi ya ujenzi, Wahandisi wa Halmashauri zote wamebaisha kuwa ipo miradi iliyokamilika, ambayo haijakamilika na Ile iliyoko katika hatua za mwisho huku wakibainisha changamoto wanazokumbana nazo katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Kwa upande wake Mhandisi wa Manispaa ya Morogoro Juma M. Gwiso amesema kuwa miradi mbalimbali imetekelezwa katika Manispaa hiyo ikiwemo ujenzi wa shule ya sekondari kata ya Boma, ujenzi wa soko la wamachinga fire, ujenzi wa hospitali ya wilaya, ujenzi wa mabweni ya shule ya sekondari Kilakala, ujenzi wa bwalo la chakula Fungafunga, ujenzi wa kituo cha afya kata ya Tungi, ujenzi wa madaraka manner shule ya sekondari Morogoro na ujenzi wa Barabara zenye urefu wa kilometa 12.85

Naye muwasilishaji kutoka katika Halmashauri ya wilaya ya Morogoro Vijijini ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa Divisheni ya Miundombinu wa Halmashauri hiyo Juma Chimwaga amesema kuwa Halmashauri ilipokea shilingi bilioni 8.9 Kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo huku miradi kadhaa ikiwa imefikia asilimia 90 ya ujenzi. Amesema kuwa zipo changamoto kama vile ukosefu wa usafiri na na upungufu wa wataalam u wa ujenzi jambo linalopelekea kuchelewa kukamilika Kwa baadhi ya miradi.

Halmashauri nyingine zilizopata nafasi za kuwasilisha  utekelezaji wa miradi ya ujenzi ni pamoja na Halmashauri ya Ifakara Mji, Halmashauri ya Ulanga, Halmashauri ya Kilosa, Halmashauri ya Mlimba, Halmashauri ya Mvomero, Halmashauri ya Gairo na Halmashauri ya Malinyi.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa