• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WAJASIRIAMALI WADOGO WADOGO WAHAMASHISHWA KUCHUA VITAMBULISHO - DC

Posted on: February 25th, 2019

Machi 25 mwaka huu Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi ametoa wito kwa wajasiriamali wadogo wadogo wasiozidi kipato cha milioni nne kwa mwaka kuhakikisha wanakuwa na vitambulisho vya wajasiriamali wadogo wadogo vitambulisho ambavyo vimetolewa na Mheshimiwa Rais lengo ikiwa ni kuwajali wajasiriamaqli hao ambapo wilaya ya Kilosa mpaka sasa imepokea jumla ya vitambulisho  9500.

Mgoyi ametoa wito huo wakati wa kampeni ya kuhamasisha wajasiriamali hao kuchukua vitambulisho hivyo katika tarafa ya Magole kwa kata za Msoero, Dumila, Mvumi,Magole na Kitete ambapo licha ya kutoa hamasa lakini pia aligawa vitambulisho kwa wajasiriamali wa Dumila na Feri-Magole waliojitokeza kuchukua vitambulisho hivyo vinavyopatikana kwa shilingi 20,000/=.

Akielezea kuhusu vitambulisho hivyo Mgoyi amesema kuwa vinampa fusra mjasiriamali     kufanya biashara ya aina yoyote isiyozidi millioni nne kwa mwaka eneo lolote hapa nchini lakini pia kinamsaidia kufanya biashara eneo lolote kwa uhuru huku akiaminika katika maeneo atakayofanyia biashara kupitia uwepo wa kitambulisho hicho.

Aidha amewataka watendaji wa kata, watendaji wa vijiji pamoja na wenyeviti wa vijiji kuongeza kasi ya uhamasishaji na kuwatambua wajasiriamali wanaostahili vitambulisho ili waweze kupatiwa huku akiwasisitiza wafanyabiashara mbalimbali kuwa yapo makundi mawili ambayo ni mfanyabiashara kuwa na namba ya mlipa kodi TIN au kuwa na kitambulisho cha mjasiriamali na kwamba kila mfanyabiashara lazima awe na utambulisho kati ya TIN au kitambulisho na kwa atakayebainika kutokuwa na utambulisho wowote hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Akibainisha aina za biashara na wajasiliamali wanaostahili kupata vitambulisho Mtendaji wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kilosa Reginald Simba amesema wajasiriamli wanaostahili kuwa na vitambulisho ni mama/baba lishe, boda boda, wasusi wa nywele, vinyozi, mafundi viatu, wauza CD na kanda za video, wanaoingiza nyimbo kwenye memory card, wakaanga chips, wauza mbogamboga, waosha magari, wapaka rangi kucha, wauza dawa za mbu na za asili, wakodishaji baiskeli, wauza maji,soda, mafundi seremala, wasukuma maguta/mikokoteni, wauza matunda,mafundi saa au simu, watembeza biashara mikononi na wengine wenye biashara kama hizo.

Licha ya kufanya hamasa katika tarafa ya Magole Mgoyi ametembelea shule za Sekondari Dumila na kujionea ujenzi unaoendelea wakati huo huo diwani wa kata ya Kitete Mh. Steven Lugome akitoa ombi kwa Mkuu wa Wilaya kutembelea shule ya Sekondari Kitete kujionea ujenzi wa madarasa mawili na ofisi unaoendelea na kuwaunga mkono ambapo Mkuu wa Wilaya huyo ametembelea shule hiyo na kutoa ahadi ya kuchangia mifuko 20 ya saruji.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa