• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WAJIBIKENI KWA MUJIBU WA MAJUKUMU YENU

Posted on: September 18th, 2018

Maafisa Tarafa, Watendaji wa Kata na Vijiji wilayani Kilosa wametakiwa kutambua vema majukumu yao licha ya uwepo wa ugumu na changamoto mbalimbali zilizopo ambazo haziwaondolei watumishi hao wa umma  kufanya majukumu yao ipasavyo kwani wameaminiwa na serikali kuwepo kwa maeneo ya kazi, hivyo wanapaswa kufanya majukumu yao kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni za kazi ikiwemo kuwasimamamia kimajukumu watumishi walio chini yao kwa mujibu wa misingi ya utawala bora kwa kuhakikisha wanafanya majukumu yao ipasavyo kwa kuwahudumia wananchi.

Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale wakati wa kikao cha Mkurugenzi huyo kilichoshirikisha Wakuu wa Idara na Vitengo, Maafisa Tarafa, Watendaji wa Kata na Vijiji ambapo amewataka watumishi hao kusimamia na kukusanya mapato ya Halmashauri  kwa kuzingatia uadilifu katika ukusanyaji mapato kwa kusimamia maadili ya utumishi wa umma pamoja na utoaji takwimu sahihi na taarifa muhimu kwa wakati kwa maslahi ya Halmashauri na Taifa kwa ujumla.

‘‘Aidha niseme kuwa Maafisa Tarafa, Watendaji wa Kata na Vijiji mnao wajibu wa kusimamia miradi ya maendeleo ili ijengwe kwa ubora na ikamilike  kwa wakati ili wananchi wapate  huduma wanazostahili kwani usimamizi wa miradi ni sehemu ya majukumu yenu ikiwemo utoaji wa taarifa za mara kwa mara kwa viongozi wa juu kwa kila kinachoendelea hasa katika miradi jambo litakalosaidia Halmashauri kutokuwa na hoja zinazoashiria ubadhirifu wa fedha na maswali ya sintofahamu pindi ziara mbalimbali za viongozi zinapojitokeza pamoja na utoaji huduma bora kwa wananchi bila ya ubaguzi, upendeleo wala viashiria vya rushwa’’. Ameongeza Mwambambale.

Aidha katika kikao hicho Wakuu wa Idara walitoa mada mbalimbali kwa watendaji hao lengo ikiwa ni kuwakumbusha majukumu yao kama watumishi wa umma ambapo miongoni mwa mada hizo ni Uwajibikaji na usimamizi wa mapato, Kuzingatia Dhana ya Utawala bora katika uwajibikaji kwa wananchi, Udhibiti na utatuzi wa migogoro ndani ya jamii na kwa wananchi, Uanzishwaji, utunzaji na uhuishaji wa daftari la wakulima, Kampeni ya ujenzi wa vyoo bora kwa afya bora katika jamii, Uhifadhi na utunzaji wa mazingira na kuepuka athari za uharibifu wa mazingira.

Mada nyingine ni Usimamizi wa vibali vya ujenzi na kuzuia ujenzi holela, Kuanzisha na kuhuisha Rejista za wakazi kwenye vitongoji, Maelekezo na maagizo ya Serikali na Halmashauri, Jumuiya za watumia maji vijijini pamoja na Sheria ndogo, Mikataba na Mabaraza ya kata ambapo mwanasheria wa Halmashauri amewataka watendaji hao kutambua kuwa jukumu la kuandaa mikataba ni la Ofisi ya sheria hivyo linapaswa kuzingatiwa ili kuepuka athari mbalimbali zinazoweza kujitokeza ikiwemo kukiukwa kwa taratibu na kanuni za mikataba mbalimbali pamoja na kuepuka kesi ambazo zinazoweza kujitokeza dhidi ya Halmashauri.

Katika kuhitimisha kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji amewaagiza watendaji wote kuainisha vyanzo vyote vya  mapato katika maeneo yao pamoja na kuainisha uwezo wa kila chanzo sambamba na kufufa akaunti zote za vijiji ili 20% zinazopaswa kurudishwa katika vijiji kwa mujibu wa sheria ziweze kurudishwa kupitia akaunti hizo kwa ajili ya kufanya maendeleo katika vijiji.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa