• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WAJUMBE WA BODI YA AFYA WATAKIWA KUZINGATIA MAJUKUMU YAO KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA-DC KILOSA

Posted on: November 8th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi ametoa wito kwa wajumbe wa bodi ya afya Wilaya kuzingatia wajibu na majukumu yao katika kuboresha huduma za afya na kutenda haki kwa kila mtu na kutoa maamuzi sahihi kwa muda sahihi ili mwisho wa siku tuungane pamoja na serikali katika kuboresha huduma za afya na kwamba ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, itaendelea kutoa ushirikiano kwa kufanya kazi kwa karibu na bodi.

Mgoyi amesema hayo wakati wa uzinduzi wa bodi ya afya Wilaya ambapo amesema kuwa  Bodi na Kamati za vituo vya kutolea huduma za afya zipo kwa mujibu wa sheria na zina majukumu mbalimbali ya kutekeleza ikiwa ni pamoja na kujadili na kurekebisha mipango ya Afya na Bajeti na kuziwasilisha Halmashauri ili iidhinishwe.

Aidha amesema bodi inao wajibu wa kupokea, kuchambua na kuidhinisha taarifa za Utekelezaji shughuli za idara kutoka kwa timu ya Uendeshaji wa huduma za Afya ya Halmashauri (CHMT),kubuni na kushauri vyanzo mbalimbali vya mapato, na pia ameitaka bodi hiyo kushirikiana na Kamati za Afya na Washirika wengine kwa kuinua kiwango cha utoaji huduma ya Afya  na kuwa na uhusiano wa kiutendaji na kamati za usimamizi za Vituo na kwamba haitangilia mambo ya kitaalamu ya Watumishi katika maadili ya kikazi.

Pia ameitaka bodi hiyo kuwa chachu ya ufanisi ya kuhakikisha huduma za afya ziko vizuri na pindi zinapopata malalamiko zisiamini kabla ya kuona hivyo pindi zinapopokea malalamiko zifanye ufuatiliaji ili kubaini ukweli wa jambo husika pamoja kusimamia uboreshwaji huduma za afya katika vituo vya afya sambamba na kuongeza kasi ya uhamasishaji kwa wananchi kujiunga na mfuko wa bima ya afya CHF kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia kupata ongezeko la mgawanyo wa dawa katika Wilaya.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Afya Dkt. Fred Mwanyesya amesema kuwa kila mmoja awajibike kwa nafasi yake na kutofanya kazi kwa mazoea ili kuleta mabadiliko katika Wilaya ya Kilosa na ameahidi wao kama bodi wataendeleza mabadiliko yaliyopo ikiwemo kuhamasisha wananchi kujiunga na CHF lakini pia kusaidia kuongeza na kusimamia vyanzo vingine vya mapato ikiwemo kusimamia rasilimali za vituo vya afya na kutilia mkazo upatikanaji wa watumishi wa afya  sambamba kutofanyia kazi majungu bali iko tayari kufanyia kazi mambo yaliyo na ukweli.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa