• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

wakaguzi wa mazingira toeni ushauri badala ya adhabu RC Morogoro.

Posted on: May 13th, 2018

Wakaguzi wa Mazingira Kanda ya Mashariki inayojumuisha Mikoa ya Pwani, Tanga na Morogoro wametakiwa kujikita katika kutoa ushauri wa Kitaalamu juu ya suala nzima la uharibifu wa mazingira badala ya kufikiria zaidi kutoa adhabu.

Rai hiyo imetolewa hivi karibuni na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe kupitia hotuba yake iliyosomwa na Katibu Tawala wa Mkoa huo Bw. Clifford Tandari wakati akifungua mafunzo ya wakaguzi wa mazingira Mikoa ya Morogoro, Tanga na Pwani yaliyofanyika chuo kikuu cha sokoine, Mjini Morogoro.

Dkt. Kebwe amesema pamoja na kuwa Wakaguzi hao wana kazi ngumu na inayohitaji umakini lakini pia Wakaguzi hao (environmental inspectors) wametakiwa kufanya kazi zao kwa weledi mkubwa ikiwa ni pamoja na kukjikita katika kutoa ushauri zaidi pindi wanapoona kuna uvunjifu wa sheria za mazingira na kwamba hatarajii kusikia wanatoa adhabu, bila kwanza kutoa ushauri wa kitaalam. Alisema Dkt. Kebwe.

Aidha, Dkt. Kebwe amesema Viongozi wa Mikoa ya Kanda ya Mashariki wanaamini kuwa kwa Kuteuliwa Wakaguzi hao wa Mazingira na kwa madaraka makubwa waliyopewa na Mhe. Waziri mwenye Dhamana ya Mazingira hawatarajii kuona au kusikia matukio ya uharifu wa mazingira kwenye Mikoa yao na kuwa katika mkoa wa Morogoro hatakubali kusikia uharibifu wa mazingira unatokea katika maeneo ambayo mkaguzi wa mazingira yupo.

Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa amewaasa Wakaguzi hao kuelewa kuwa kwa sasa nchi inaelekea kwenye uchumi wa viwanda, hivyo wanatakiwa kuwasaidia wawekezaji kuwekeza na kuzalisha bidhaa bila kuharibu mazingira yaliyopo.

Awali, akimkaribisha Mgeni Rasmi kufungua mafunzo hayo, Mratibu wa Mazingira Kanda ya Mashariki Bw. Japhari Chamgege alisema Wakaguzi wa Mazingira wameteuliwa na Waziri kwa mujibu wa sheria ya Usimamizi wa Mazingira, Kifungu cha 182 (1) & (2) kinachompa Waziri mwenye dhamana ya Mazingira mamlaka ya kuteua Wakaguzi wa Mazingira miongoni mwa mtumishi kutoka mamlaka za Serikali za mitaa, Wizara au Asasi yoyote ya umma.

Chamgege amesema kutokana na sheria hiyo Mhe. Waziri amekwisha teua Wakaguzi wa Mazingira 471 kote nchini na kufanya idadi ya Wakaguzi hao kufikia 500 ukijumuisha na Wakaguzi wa Mazingira waliokuwepo kabla ya Uteuzi huo.

Aidha, Mratibu huyo wa Mazingira alibainisha majukumu ya Wakaguzi hao wa Mazingira kuwa ni pamoja na kuingia kwenye jengo lolote, ndani ya gari, ndege, chombo cha majini, ardhi au mahali pengine pasipo kuwa na makazi ya kawaida ya watu ili kufanya ukaguzi.

Majukumu mengine ni kusimamisha gari au chombo chochote cha majini au ardhini ambacho wanaamini kwa dhati kuwa chombo hicho kinaendeshwa na kinamwaga au kimekwishamwaga kitu chochote kinachochafua mazingira kinyume cha sheria hii au, kukamata au kuzuia shughuli yeyote inayoharibu mazingira.

Mmoja wa Wakaguzi wa Mazingira Walioteuliwa na Waziri mwenye Dhamana, Bw. Venance Segere ambaye ni Afisa Mazingira kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, amesema anashukuru kwa uteuzi huo kwani unampa nguvu ya kufanya kazi kwa bidii zaidi kwa kuwa ameaminika na Serikali. Aidha, amesema warsha hiyo imekuja wakati mwafaka kwao na watatumia utaalamu wao na vipaji kwa uaminifu kwa ajili ya kuwasaidia watanzania wenzao ili waweze kuishi katika mazingira bora zaidi.



Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa