• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Wakazi wa kijiji cha Chabima mbioni kupata huduma za afya katika zahanati ya Chabima

Posted on: February 4th, 2022

Wakazi wa Kijiji cha Chabima kilichopo kata ya Masanze wilayani Kilosa wamekuwa wakitembea umbali wa kilomita 35  tangu kuanzishwa kwa kijiji hicho ili kuweza kufika hospitali ya wilaya ya Kilosa ili kupata huduma za kiafya.

Hayo yamebainishwa Februari 3 mwaka huu kijiji hapo wakati Kamati ya CCM Wilaya ilipotembelea Mradi wa Mkaa endelevu na ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Chabima ambapo imebainishwa kuwa wakazi wa kijiji hicho hutembea umbali mrefu ili kupata huduma za kiafya jambo lililopelekea kijiji hicho kuazimia kujenga zahanati ili iweze kuwasaidia kupunguza adha yakutopatikana kwa ukaribu kwa huduma hizo.

Akisoma taarifa hiyo mjumbe wa kamati ya maliasili ya kijiji cha chabima Idd Tangula amesema kuwa kijiji hicho kimeanzishwa mwaka 1973 na hakukuwa na zahanati kwa kipindi chote hadi mwaka 2012 ndio ulianza ujenzi wa zahanati inayogharimu milioni 120 ambayo imekamilika kwa nguvu kazi za wananchi,halmashauri ikiwa imetoa milioni 32 na Mwenyekiti wa CCM Wilaya Mh. Ameir Mubarak akitoa mifuko 50 ya saruji na kwamba kwasasa wanamalizia ujenzi wa choo.

Aidha amesema kuwa licha ya kukamilika kwa ujenzi huo bado wanakabiliwa na changamoto ya samani za ofisi, vifaa tiba, bomba la maji na daktari hivyo wameiomba Serikali kuwasaidia ili waweze kuepukana na adha hiyo ambayo inagharimu maisha ya watu hususan wajawazito na watoto chini ya miaka mitano.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilosa ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya Alhaj Majid Mwanga ameonyesha kutoridhishwa na gharama za ujenzi ambazo hazilingani na ubora wa jengo uliopo ambapo imetumika zaidi ya milioni 86 mpaka sasa.

Mwanga licha ya kasoro zilizopo katika ujenzi huo unaoendelea ameitaka Serikali ya kijiji kuhakikisha ujenzi huo unakamilika mara moja na fedha ambayo ipo itumike katika ununuzi wa vitanda vya kujifungulia wazazi ili wananchi waanze kupatiwa matibabu kijijini hapo huku akiahidi kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kuhakikisha daktari anapatikana ujenzi utakapokamilika ambapo pia amewahamasisha wananchi hao kuchukua tahadhari dhidi ya Uviko-19 kwa kupata chanjo ya Uviko 19.


Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • ZABUNI January 31, 2017
  • SOMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA March 24, 2017
  • UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA March 24, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • Kilosa kufanya sensa ya mifugo

    December 29, 2022
  • Kilosa kunufaika na mradi wa BOOST

    December 24, 2022
  • Kilosa yaendelea kutambua juhudi za Serikali kwa Watumishi wa Umma na Wananchi-DED Kilosa

    December 19, 2022
  • -Serikali haitosita kulinda Rasilimali watu kwa maslahi ya Maendeleo ya Taifa- Mh. Mhagama

    December 20, 2022
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa