• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WAKINA MAMA WANAONYONYESHA WILAYANI KILOSA WAMEASWA KUZINGATIA MLO BORA ILI WATOTO WAPATE VIRUTUBISHO MUHIMU KUPITIA MAZIWA YA MAMA

Posted on: August 6th, 2025

Maadhimisho ya Wiki ya Unyonyeshaji Duniani yamefanyika leo Agosti 6, 2025 katika viwanja vya Kliniki ya Mama na Mtoto wilayani Kilosa, yakilenga kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa lishe bora na mazingira rafiki kwa mama mnyonyeshaji.

Afisa Lishe wa Wilaya, Jackson Kalibwani, ameeleza kuwa lishe bora kwa mama anayenyonyesha ni nguzo ya kwanza ya kuhakikisha mtoto anapata maziwa ya kutosha na yenye virutubisho muhimu.

Aidha amesisitiza ulaji wa makundi yote sita ya chakula, akibainisha kuwa hali ya lishe duni kwa mama huathiri moja kwa moja ukuaji wa mtoto, pia amewashauri wanafamilia kushirikiana katika kumsaidia mama mnyonyeshaji kimazingira na kihisia.

Naye Mratibu wa huduma za mama na mtoto, Bi. Prisca John amesema kuwa unyonyeshaji wa maziwa ya mama pekee kwa miezi sita ya mwanzo ni silaha madhubuti dhidi ya vifo vya watoto wachanga ambapo pia ameeleza umuhimu wa chanjo kwa watoto kama sehemu ya kuhakikisha afya bora, huku akisisitiza wajibu wa wazazi kufuatilia huduma hizo kwa karibu.

Kwa upande wake Mgeni rasmi Odilia Haibei akimwakilisha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kilosa, amehimiza ushirikiano wa serikali na wadau kama Compassion na World Vision katika kuhakikisha elimu ya lishe na afya inawafikia wananchi wote, hasa walioko vijijini huku akiwataka wakazi wa Kilosa kutambua kuwa uwekezaji katika lishe na mazingira salama ya unyonyeshaji ni uwekezaji kwa taifa lenye afya na uwezo wa kiuchumi.

Kauli mbiu ya mwaka huu “Thamini Unyonyeshaji; Weka Mazingira Wezeshi kwa Mama na Mtoto” imekuwa kiini cha mafunzo na elimu kwa wakazi wa Kilosa.

Tangazo

  • TANGAZO LA MAFUNZO YA UDEREVA WA MAGARI, PIKIPIKI NA BAJAJI September 30, 2025
  • TANGAZO LA TOZO September 10, 2025
  • TANGAZO LA KUKODISHA MASHAMBA YA HALMASHAURI September 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA DARASA LA SABA November 23, 2023
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • WANANCHI WILAYANI KILOSA WAHIMIZWA KUFANYA UCHUNGUZI WA AWALI WA SARATANI YA MATITI

    October 01, 2025
  • WASIMAMIZI WA MIRADI NGAZI YA SHULE WATAKIWA KUFANYA TATHMINI KWA KILA HATUA YA UJENZI

    September 28, 2025
  • KILOSA YAFANIKIWA KUCHANJA MBWA WENGI KATIKA WIKI YA KICHAA CHA MBWA

    September 28, 2025
  • WANANCHI WA KIJIJI CHA MAGUHA KUNUFAIKA NA MASHINE YA KUCHUJA ASALI

    September 21, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa