• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WAKULIMA NA WAFUGAJI WAASWA KUWA NA MARIDHIANO - DC

Posted on: February 26th, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa adam mgoyi ameitaka jamii ya wakulima na wafugaji kuwa na hulka ya maridhiano hasa katika matumizi ya ardhi kwani kila mtu anayo haki ya kuishi na kutumia ardhi kwa kufuata taratibu na kutenga maeneo kwa kadri ya matumizi kulingana na shughuli zao kwani jamii zote mbili ni watanzania ambao wana haki ya kufanya shughuli zao kwa uhuru kwa kufuata taratibu.

Mgoyi amesema hayo Machi 26 mwaka huu alipotembelea kijiji cha Mfulu yalipotokea mauti ya  mkulima ambapo amesema kuwa watendaji wa kata wanao wajibu wa kushirikiana na viongozi wa vijiji na kupanga maeneo kwa matumizi mazuri na kuhakikisha lazima kuwepo na njia kwa ajili ya kupita mifugo badala ya kulima maeneo yote kwani kutokuwepo kwa njia za mifugo kutasababisha migogoro ikiwemo mapigano ya wakulima na wafugaji.

Akizungumzia kuhusu kifo cha mwanamke aliyefariki maeneo hayo Mkuu wa Wilaya amesema hadi sasa chanzo cha kifo cha mama huyo bado hakijafahamika na kwamba hatua zilizochukuliwa baada ya tukio hilo ni kuupeleka mwili wa mama huyo hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa ajili ya uchunguzi, hivyo amewataka wananchi hao kuwa watulivu mpaka hapo taarifa za uchunguzi wa kidaktari zitakapotolewa kubainisha chanzo cha kifo hicho.

Aidha mgoyi amesema kwa sasa hakuna kijiji cha Mabwegere kwa mujibu ripoti iliyotolewa na mchunguzi kwani hati ya awali iliyotolewa kwa kijiji hicho iligubikwa na dhuluma na kwamba kwa sasa mwenye mali kwa eneo hilo ni Mkurugenzi Mtendaji na kwamba eneo hilo litatambulika rasmi mara baada ya kukamilika kwa taratibu zote za uchorwaji upya wa ramani kwani kwa sasa ramani ya iliyokuwa Mabwegere haitambuliki mpaka hapo vijiji vitakapotengwa upya kwa kufuata taratibu ambapo kwa sasa eneo hilo liko chini ya kijiji mama cha Mfulu.

Naye Mrakibu Msaidizi wa Polisi Daud Nkuba amesema kuwa baada ya kupata taarifa walifika eneo la tukio wakiwa wameambatana na daktari na kufanya uchunguzi wa awali kujua chanzo cha tatizo na kwamba kwa upande wa Jeshi la Polisi wamefanya mahojiano na baadhi ya wakazi wa eneo hilo ili kufatilia wanaodaiwa kuhusika na tukio hilo ambapo inadaiwa kuwa mkulima huyo ajulikanaye kama Asha Shomari (56) mkazi wa Morogoro baada ya kuona ngombe wameingia shambani kwake ambalo mpunga ndio umeanza kuchipua alikimbilia shambani humo kwa lengo la kuzuia ndipo alipokumbwa na umauti.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa