• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WAKULIMA TAMBUENI FURSA NA KUZITUMIA

Posted on: January 25th, 2020

Fursa mbalimbali hujitokeza kutokana na njia mbalimbali ikiwemo changamoto za jamii, kuanzishwa kwa miradi mikubwa katika maeneo jamii inakoishi, kuongezeka kwa idadi ya watu, kuvumbuliwa kwa rasilimali ya asili kama vile madini, gesi nk au kukua kwa uchumi wa jumla ambapo watu huweza kutumia njia hizo kufanya shughuli za kujiongezea kipato kwa njia ya biashara.

MENEJA URASIMISHAJI RASILIMALI ARDHI VIJIJINI ANTHONY TEMU

Hayo yamebainishwa Anthony Temu Meneja Urasimishaji Rasilimali Ardhi Vijijini kutoka MKURABITA wakati wa mafunzo kwa wakulima waliorasimisha ardhi zao na kupata hati miliki katika kijiji cha Magubike katika kata ya Magubike juu ya masuala mbalimbali ya kilimo, uthaminishaji ardhi na ushirika ambapo upande wa kutafuta fursa Temu amesema utafutaji fursa na namna ya kuzitumia jamii inapaswa kuzitambua vema fursa na kuchukua hatua ya uthubutu katika kufanya michakato mbalimbali ili kuboresha kipato na kuinua ufanisi na kujiwezesha kiuchumi kutokana na ujasiliamali kwani ujasiliamali ni kuwa na mshawasha wa kutafuta na kupata mali kwa kutambua fursa mbalimbali za biashara.

DIWANI WA KATA YA MAGUBIKE MH. CHILOLO AKIWA MMOJA YA WASHIRIKI WA MAFUNZO, 2 & 3 BAADHI YA WASHIRIKI WA MAFUNZO HAYO KATIKA KIJIJI CHA MAGUBIKE


Temu amesema jamii inaweza kutambua fursa kupitia mambo makubwa matatu ambayo ni motisha utokanao na kutafuta fursa kwa sababu kuna motisha katika kufanya jambo husika, msukumo na namna gani ya kufikia fursa hizo ambapo amesema mambo mengine ya kuzingatia ni ufuatwaji wa sheria na taratibu za fursa husika, kuzingatia hali halisi ya eneo husika, kuzingatia mwenendo wa maisha  ya wakazi wa eneo husika  na mfumuko wa bei aidha amesema kuwa fursa zinaweza kutumika kwa kuangalia namna ya upatikanaji wa huduma unayotaka kutoa, idadi ya ushindani wanaotoa huduma husika, matakwa ya wateja katika eneo na idadi yao pamoja na gharama za uendeshaji wa biashara ambapo pia amesema utafutaji wa fursa utaleta maendeleo ya haraka kiuchumi, huku ubunifu ukiongeza shughuli za aina mbalimbali katika jamii na kuongeza ufanisi pamoja na kupanua soko.

MTHAMINI WA ARDHI BW. LIBERATUS AKITOA ELIMU YA UTHAMINISHAJI WA ARDHI

Naye Mthamini toka Idara ya Ardhi Wilaya ya Kilosa Bw. Liberatus Modest amesema kuwa ardhi inaweza kutumika kujiongezea kipato kwa kuiongezea thamani na ulinzi ambao ni hati miliki ambayo inasaidia katika kupata mkopo lakini pia dhamana hivyo watu wanapaswa kufahamu umuhimu wa nyaraka za ardhi na kuzitunza kwani ardhi inapaswa kuongezwa thamani kwa kuzingatia matumizi ya ardhi kwa asilimia kubwa na kutegemea nyaraka zilizopo zinazozipa ulinzi, pia matumizi ya ardhi yanachangia kwa kiasi kikubwa thamani ya ardhi kuongezeka kutokana na vilivyopo ndani ya ardhi kama vile kupanda mazao ya kibiashara yenye kudumu na ushindani katika soko kama minazi nk lakini pia kujenga nyumba ya kudumu na yenye viwango mfano makazi na biashara.

AFISA USHIRIKA BI ROSE AKITOA ELIMU YA USHIRIKA


Akizungumzia umuhimu wa ushirika Afisa Ushirika Wilaya Rose Matemba amesema kuwa na chama cha ushirika kunawezesha wanaushirika kuwa na uhakika wa mahali pa kukusanyia bidhaa zao wakati wakisubiri bei nzuri ya uhakika wa soko, kutoa fursa inayomwezesha mwanaushirika kushiriki katika uchumi wa jamii anamoishi, kuwawezesha kukopesheka na taasisi mbalimbali za kifedha,  kuweza kupata fursa mbalimbali mfano miradi ya kilimo, pamoja na miradi mingineyo lakini pia vyama vya ushirika vinaweza kutumika kama wakala wa kukusanya ushuru.

Naye afisa kutoka benki ya NMB Kilosa Elibariki Mwambashi amewashauri wakulima kuwaza mahali pa kwenda kuuza bidhaa za kabla ya kuanza kuzalisha kwani kitendo cha kufahamu mahali pa kwenda kuuza itasaidia kwa kiasi kikubwa kujua uzalishe kiasi gani jambo linalosaidia kujua hali ya soko na kuepuka hasara zinazoweza kuepukika lakini pia wao kama benki ili kumkopesha mkulima ama kikundi ni lazima mkulima/kikundi  kitambue mahali kitakapopeleka bidhaa zake.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa