• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WAKULIMA WASHAURIWA KUWAJIBIKA KWA ENEO LAO

Posted on: June 21st, 2020

Mradi wa uwajibikaji jamii katika ufatiliaji wa rasilimali za umma ulio chini ya mtandao wa wakulima wadogo Tanzania unaofadhiliwa na SDC katika uboreshwaji na utolewaji wa huduma za ugani kupitia maafisa ugani ambao watakuwa wakitoa elimu kwa wakulima kwa mbinu za kiikolojia kwa kuhakikisha huduma za ugani ili kukabiliana na changamoto mbalimbali za kilimo hivyo kuwasaidia wakulima hususani wanawake kwa kuboresha huduma za ugani.

Hayo yamebainishwa na Mratibu wa MVIWATA kanda ya kati Morogoro Joseph Sengasenga ambapo amesema mradi huo wa miaka minne utafanya kazi katika vijiji vitano vya Mhenda, Ilonga, Ulaya, Madudu na Rudewa Gongoni ambapo amesema mradi huo unalenga suala zima la uwajibikaji baina ya wapokea huduma ambao ni wakulima na watoa huduma ambayo ni Serikali ambapo huduma zitakazotolewa zinalenga katika kuboresha maisha ya jamii nzima ambapo jamii na Serikali kila moja kwa eneo lake akiwajibika italeta matokeo chanya katika sekta ya kilimo na kuleta tija kwa Serikali kwa kukusanya mapato huku jamii ikifaidika na utatuzi wa changamoto zinazowazunguka.

Akizungumzia maazimiao yaliyofikiwa baada ya matumizi ya pima kadi iliyofanyika katika vijiji hivyo ili kubaini changamoto na mapendekezo yaliyojitokeza Sengasenga amesema imebainika kutokuwepo kwa mashamba darasa katika baadhi ya vijiji ambayo yanapaswa kuanzishwa ili kueneza ujuzi na maarifa ya kilimo cha mazao tofauti tofauti kwa wakulima jambo litakalosaidia wakulima kulima kwa tija.

Naye kaimu mkuu wa wilaya Reginald Simba ametoa rai kwa wakulima kutambua kuwa serikali haifanyi kazi peke yake bali inafanya kwa kushirikiana na wadau m,mbalimbali hivyo amewataka wakulima mbalimbali wilayani kilosa kutumia kwa tija fursa ya uwepo wa wadau mbalimbali na kuendeleza jitihada za serikali sambamba na za wadau mbalimbali kwa kuendeleza mema yoteb yanayotolewa na wadau hao ili kuendelea kupata tija.

Simba amesema ni vema wanakilosa wakawa mstari wa mbele katika kufikia malengo kwa kuhakikisha wanaepukana na kilimo cha mazoea ambapo kimekuwa kikifanyika kwa muda mrefu na kusababisha kudumaa kimaendeleo kwani hulka ya kutobadilika ni kikwazo cha kutosonga mbele hivyo ni vema kuwatumia watalaam na kwamba maendeleo yanaanzia kwa mtu mmoja mmoja kwa kushirikiana na Serikali.

Pamoja na hayo Simba amesema anategemea kuwa kupitia mradi wa MVIWATA wakulima hao watapiga hatua na kubadili fikra zao kwa kuziangalia changamoto zinazowakabili kama fursa na kuzitafutia ufumbuzi ambao uko ndani ya maeneo yao hivyo ili kuzikabili changamoto hizo ni vema wakajipanga namna ya kuzikabili na kuzipatia majibu stahiki ikiwemo suala la ujazo wa lumbesa ambao wakulima wakiweka nia na msimamo wa pamoja kutouza mazao kwa lumbesa jambo ambalo linawezekana.

Naye Afisa Utumishi na Utawala Noel Abel akizungumzia upande wa changamoto ya kutofanyika kwa vikao vya kisheria amesema viongozi wa vijiji wanakumbushwa kuhakikisha vikao vya kisheria vinafanyika inavyostahiki na kwamba kamati ya huduma za jamii inao wajibu wa kuweka ajenda za changamoto za wakulima kama vile ugawaji ardhi na kutenga maeneo lakini pia ipo haja ya halmashauri ya kijiji kusimamia matumizi ya ardhi, ufugaji na masuala mbalimbali ya wakulima hivyo halmashauri ya kijiji isimamie uanzishwaji wa shamba darasa kwa ajili ya wakulima. 

 

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa