• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WAKUU WA SHULE NA MA-AEK WATAKIWA KUINUA UFAULU SHULENI

Posted on: February 18th, 2025

Wakuu wa Shule za Sekondari pamoja na Maafisa Elimu Kata wametakiwa kusimamia elimu ili kufikia malengo ikiwa ni pamoja na kukuza ufaulu kwa kiwango cha daraja la kwanza, la pili na la tatu lakini pia kupunguza kiwango cha wanafunzi wanaofeli.

Wito huo umetolewa na Afisa Elimu Taaluma kutoka Divisheni ya Elimu Sekondari Millandu Kinyonga wakati akizungumza na wakuu wa shule za sekondari pamoja na Maafisa Elimu Kata katika kikao kazi kilichofanyika 18 Februari, 2025 katika ukumbi wa Mamboya.

Bi. Millandu amefafanua kuwa malengo ya Halmashauri katika upimaji wa kidato cha pili na kidato cha nne kwa mwaka 2025 ni kufuta daraja sifuri na kuhakikisha kuwa kila mwanafunzi anayemaliza kidato cha nne anapata cheti lakini pia kupunguza ufaulu wa daraja la nne na kuongeza ufaulu bora yaani daraja I, II, na III.

Aidha ameongeza kuwa pia Halmashauri inalenga kuboresha miundombinu ya ufundishaji ili kuhakikisha kila shule inafikia asilimia 100 ya ufaulu.

Akiwasilisha taarifa ya matokeo ya mtihani wa taifa wa kidato cha pili na kidato cha nne kwa mwaka 2024, Daniel Kisoso ambaye pia ni Afisa Elimu Taaluma amefafanua kuwa asilimia 79 ya wanafunzi wa kidato cha pili waliopimwa walifaulu ikiwa ni ongezeko la asilimia 02 kulinganisha na matokeo ya upimaji wa mwaka 2023.

Ameongeza kuwa kwa kidato cha nne, wanafunzi 3882 wamefaulu mtihani ikiwa ni sawa na asilimia 90.2 ya waliofanya mtihani na kuongeza kuwa ufaulu huo umepanda kwa asilimia 08 kulinganisha na matokeo ya mtihani wa mwaka 2023 na kuifanya Halmashauri kushika nafasi ya nne Kimkoa.

Katika hatua nyingine, amewapongeza wakuu wa shule ambao shule zao zimefanya vizuri na kuwataka kuziendeleza jitihada hizo huku akiwataka wakuu wa shule ambazo hazikufanya vizuri kuongeza jitihada ili wapate matokeo mazuri katika mitihani inayofuata.

Naye Katibu Msaidizi Tume ya Utumishi wa Walimu Daud Mchillu amewataka wakuu wa shule pamoja na Maafisa Elimu Kata kusimamia nidhamu shuleni ikiwa ni pamoja na kuzuia utoro wa wanafunzi pamoja na walimu ili kuinua taaluma kwani vitendo hivyo huathiri tendo la ufundishaji na ujifunzaji.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa