• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WAKUU WA SHULE WASIOFAULISHA KUCHUKULIWA HATUA - RC MOROGORO

Posted on: January 16th, 2020

Walimu wakuu wa shule za sekondari wameagizwa kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa kuingia kidato cha kwanza mwaka 2020 wanaripoti shuleni na kuanza masomo mara moja kwani shule zimeshafunguliwa tangu tarehe 06/01/2020.

Agizo hilo limetolewa Januari 16 mwaka huu na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro  Loata Ole Sanare katika kikao chake na watumishi mbalimbali ambapo amewataka walimu kuhakikisha wanafunzi wanaripoti na kuanza masomo huku akizitaka shule zote zilizopokea pesa kutoka serikalini za kusapoti elimu zihakikishe fedha hizo zinatumika inavyostahiki na kwamba ukaguzi utafanyika ili kuona kama zimetumika katika usahihi lakini pia ametaka kuwepo kwa tathmini ya elimu kila wilaya ambayo itakuwa ijadiliwa na kuchukuliwa hatua stahiki.

Aidha katika kikao hicho amehoji hatua gani zilizochukuliwa kwa walimu ambao shule zao zimeonyesha kuwa na matokeo mabaya na kushika nafasi za mwisho ambapo pia amesema mwalimu yoyote ambaye hataonyesha mabadiliko katika kupandisha ufaulu anapaswa kuondolewa katika nafasi ya ukuu wa shule huku akiagiza kuondolewa kwa mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Mabwerebwere ambaye ni miongoni mwa walimu ambao shule zao zimeendelea kuwa na duni katika ufaulishaji wanafunzi ikiwemo shule za sekondari Zombo, Kutukutu, Mabwerebwere na Mikumi.


BAADHI YA WATUMISHI WAKIMSIKILIZA MKUU WA MKOA


Sambamba na hayo amesema kuwa changamoto zilizoko katika shule za msingi na sekondari zitaendelea kutatuliwa lakini pia ametoa rai kwa walimu wakuu kujipima wenyewe utendaji wao wa kazi huku akimwagiza Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari kuwa na mpango wa kuanzisha madarasa ya kidato cha tano na sita kwani shule zilizopo sasa zenye kidato cha tano na sita ni chache pamoja na kuwa na program ya pamoja ya kuongeza ufaulu kwa shule za serikali na binafsi kwa kidato cha tano na sita na kwa kutunga mtihani mmoja ambao utafanywa na wanafunzi wote wa kidato cha tano na sita kwa mujibu wa madarasa yao.

Pamoja na hayo amewataka waheshimiwa madiwani kuhakikisha wanajishughulisha katika kuhakikisha kila kata inakuwa na shule ya sekondari na kwamba diwani yoyote ambaye atakuwa nyuma katika kuleta maendeleo kwenye kata yake atakuwa amepoteza nafasi ya kugombea nafsi hiyo,

Pia ameipongeza shule ya msingi mazinyungu kwa kufaulisha kwa kiwango cha juu katika matokeo ya darasa la saba na amewazawadia shilingi laki mbili ikiwa ni sehemu ya motisha  kwa juhudi walizoonyesha huku upande wa chuo cha utabibu ameitaka TANESCO kuhakikisha miundombinu iliyopo katika chuo hicho inakuwa bora ili kuepusha kutokea kwa majanga ya kuungua moto katika mabweni hayo hakujitokezi tena.


BAADHI YA WATENDAJI WA KATA WAKIMSIKILIZA MKUU WA MKOA

Licha ya maagizo hayo Sanare ameonyesha wa kusikitishwa kwake na malalamiko ya wananchi dhidi ya watendaji wa kata na vijiji kwa kutosimamia vema majukumu yao hali inayoonyesha kukosa uwajibikaji, hivyo amewataka maafisa tarafa kuhakikisha wanawasimamia na kwa yoyote atakayebainika kutowajibika katika nafasi yake hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yake.

Pia amekemea vitendo vya rushwa vinavyoendelea na kwamba taarifa hizo za rushwa zinaendelea kuchunguzwa na mtumishi yoyote wa umma atakebainika hatasita kumchukulia hatua huku akitoa onyo kwa maafisa ugani kutenda haki wanapofanya tathmini ili kuepusha kutoweka kwa amani.

 Aidha ameuagiza uongozi wa Wilaya kuwasimamia wananchi wote bila kusita na kuhakikisha haki inatendeka pasipo kujali jamii zao ambapo amesema licha ya kuwa yeye ni mmasai lakini jamii itambue kuwa yeye si Mkuu wa Mkoa wa wamasai bali Mkuu wa Mkoa wa watu wote wa mkoa wa Morogoro huku akitoa onyo kwa wakulima na wafugaji ambao wamekuwa wakisababisha migogoro kwa kutoa malalamiko ambayo hayana ukweli ndani yake.

Kwa upande wa maswala ya kifedha ametaka watumishi wote wanaodaiwa pesa( defaulters) kuchukuliwa hatua ikiwemo kurudisha pesa zinazodaiwa na amemwagiza OCD kuwakamata mara moja watumishi wanaodaiwa huku akitaka kuhakikiwa mashine zote za kukusanyia mapato za POS kupitia ili zijulikane ziko kwa watu gani na kwamba watumishi wote wanaodaiwa wakamatwe mara moja na kusimamishiwa mishahara yao mpaka watakapolipa madeni. 


Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa