• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WAKUU WA SHULE WASISITIZWA KUHAMASISHA UANDIKISHAJI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA,AWALI NA MSINGI

Posted on: January 10th, 2024

Wakuu wa Shule Wilayani kilosa wametakiwa kuendelea kuhimiza na kuhamasisha Wazazi na Walezi kupeleka Watoto wao shule ili waweze kuandikishwa kujiunga na Elimu ya Awali na Msingi alkadhalika kidato cha kwanza  kwa wale waliopangiwa kujiunga katika shule za Umma kwani Elimu ni haki yao ya msingi na ikizingatiwa gharama za masomo zimeshalipiwa na Serikali .

Hayo yamesemwa Januari 8 2024 na Kaimu Afisa Elimu Msingi Richard Mpumilwa ambaye pia ni Afisa Elimu ya watu wazima wakati wa ziara ya kutembelea baadhi ya Shule za Msingi na awali pamoja na Sekondari zilizopo Tarafa ya Kilosa  ili kuona  mapokeo kwa siku za mwanzo baada ya kufunguliwa shule,kadhalika  hali ya uandikishaji  na mahudhurio ya Walimu na wanafunzi kwa ujumla wake  na kusema kuwa mwitikio katika baadhi ya Shule bado hauridhishi hivyo ipo haja ya kuongeza nguvu katika kuhamasisha wazazi na walezi kuleta wanafunzi shuleni, pia amewataka Wakuu wa shule  kuzingatia masuala ya usafi wa mazingira ili kuepuka magonjwa ya mlipuko.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi ambaye pia ni Mkuu wa Divisheni ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu Batuel Ruhega  amesema kuwa katika siku ya kwanza ya kufungua shule mahudhurio ya Walimu ni la lazima kwani wao ndiyo wanaoratibu mapokezi ya wanafunzi wanaokuja kujiunga katika shule zao na pia kushawishi Wazazi na Walezi kuleta wanafunzi mapema ili kuanza masomo kwa wakati  hivyo amewataka Wakuu wa Shule kusimamia  na kufuata sheria, taratibu na kanuni za kiutumishi katika utendaji wao.

Sambamba na hayo ametoa onyo kwa baadhi ya walimu ambao hawajafika katika vituo vyao vya kazi bila taarifa za maandishi na kwa sababu zisizo na mashiko na kusema kuwa watahesabika kama Watoro, pia amewataka wakuu wa shule kuwa na utaratibu wa kufanya vikao ili kuweza kujadili mambo mbalimbali ikiwemo changamoto zinazowakabili na kuweza kuzitafutia ufumbuzi kwa wakati.

Naye Katibu msaidizi wa Tume ya Utumishi ya Wlimu Daudi Mchillu amewaasa baadhi ya waalimu kuacha kuchukua mikopo kandamizi kutoka kwenye taasisi ma makampuni ya mikopo kwani hali hiyo inawasababishia madeni  hivyo kupelekea utoro kazini ambapo adhabu yake ni kubwa.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa