• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Walimu watakiwa kuendelea kuzifahamu huduma za kibenki

Posted on: August 29th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Shaka Hamdu Shaka amepongeza benki ya NMB kwa kujali mahitaji ya wafanyakazi kwa kuweka bidhaa zinazokidhi mahitaji ya makundi mbalimbali ya wafanyakazi hususani walimu ambao wamekuwa wakifaidika na mikopo nafuu na kwamba imekuwa msaada mkubwa katika kukidhi mahitaji ya familia na kuwafanya kufanya kazi kwa amani na kuleta tija katika maeneo yao ya kazi.

Shaka ametoa pongezi hizo Agosti 28 mwaka huu wakati wa warsha fupi ya “Mwalimu spesho-Umetufunza Tunakutunza” iliyowakutanisha walimu wakuu wa shule za msingi, wakuu wa shule za sekondari na walimu wa kawaida kutoka shule mbalimbali za Kilosa ambapo ametoa rai kwa walimu kutumia vizuri fursa ya elimu inayotolewa na NMB kujifunza masuala ya kibenki ikiwemo masuala ya amana, mikopo, bima na huduma mbalimbali za kibenki ambazo zitawasaidia kujenga utamadumi wa kuweka akiba ambazo zitawasaidia katika mahitaji na utatuzi wa changamoto za kifedha pindi zinapojitokeza.

Aidha ameitaka benki ya NMB kuendelea kuandaa program mbalimbali kwa makundi mbalimbali ya watumishi na wananchi kiujumla ili kuwapatia fursa ya kujua huduma zitolewazo na benki pamoja na kubuni bidhaa na huduma za kawaida ambazo mwananchi wa kawaida ataweza kuzimudu.

Pamoja na hayo amewapongeza sana walimu kwa kuunga mkono juhudi za serikali kwa kufanya kazi kwa ufanisi na kwamba wamekuwa wakifanya kazi kubwa ya kuwaandaa viongozi wa baadae na kwamba serikali itaendelea kuandaa mazingira bora kwa walimu katika kuendelea kutoa huduma bora kwa kuwawekea mazingira rafiki walimu ya kufanyia kazi na kuwa Serikali itaendelea kufanya kazi katika kuboresha maisha ya watanzania kwa vitendo.

Kwa upande wake Meneja Mwandamizi Kitengo cha Wateja Maalum Queen Kinyamagoha amesema benki ya NMB imeendelea kuja na suluhisho mbalimbali kwa makundi mbalimbali ikiwemo walimu kama njia mojawapo ya kuleta watanzania kwenye mifumo  rasmi ya kifedha na kuipatia Serikali mapato kwa kuwafikia watanzania wengi zaidi hivyo kuchangia idadi ya watanzania wanaotumia huduma za kibenki.


Pamoja na hayo kwa niaba ya NMB amesema NMB wataendelea kuja na suluhu bora na nafuu kwa watanzania  na kwamba uwajibikiaji wao kwa jamii utabaki kuwa wa viwango vya juu pamoja na kuendelea kushirikiana na Serikali katika kusukuma mbele maendeleo ya kiuchumi ya Taifa na wananchi kiujumla.

Nao walimu kwa nyakati tofauti wameishukuru benki ya NMB kwa huduma mbalimbali ikiwemo uwepo wa mikopo yenye riba nafuu inayotolewa kwa watumishi wa makundi mbalimbali kwani imekuwa msaada kwao katika kuwasaidia kujikimu kimaisha na kuwawezesha kufanya shughuli mbalimbali huku wakishukuru kwa elimu inayoendelea kutolewa na benki hiyo ambayo inawasaidia kupata uelewa zaidi juu ya huduma mbalimbali za kifedha.

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 KWA SHULE ZA SEKONDARI HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOSA July 14, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI September 16, 2023
  • ZABUNI January 31, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • KILOSA KUDUMISHA USAFI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    September 20, 2023
  • TIMU YA UKAGUZI MKOA YATEMBELEA MIRADI YA BOOST KILOSA

    September 20, 2023
  • MAPATO YA HALMASHAURI YAONGEZEKA KUTOKA ASILIMIA 94 MPAKA ASILIMIA 98.91

    September 01, 2023
  • Walimu watakiwa kuendelea kuzifahamu huduma za kibenki

    August 29, 2023
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa