• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Walimu watakiwa kuendelea kuzifahamu huduma za kibenki

Posted on: August 29th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Shaka Hamdu Shaka amepongeza benki ya NMB kwa kujali mahitaji ya wafanyakazi kwa kuweka bidhaa zinazokidhi mahitaji ya makundi mbalimbali ya wafanyakazi hususani walimu ambao wamekuwa wakifaidika na mikopo nafuu na kwamba imekuwa msaada mkubwa katika kukidhi mahitaji ya familia na kuwafanya kufanya kazi kwa amani na kuleta tija katika maeneo yao ya kazi.

Shaka ametoa pongezi hizo Agosti 28 mwaka huu wakati wa warsha fupi ya “Mwalimu spesho-Umetufunza Tunakutunza” iliyowakutanisha walimu wakuu wa shule za msingi, wakuu wa shule za sekondari na walimu wa kawaida kutoka shule mbalimbali za Kilosa ambapo ametoa rai kwa walimu kutumia vizuri fursa ya elimu inayotolewa na NMB kujifunza masuala ya kibenki ikiwemo masuala ya amana, mikopo, bima na huduma mbalimbali za kibenki ambazo zitawasaidia kujenga utamadumi wa kuweka akiba ambazo zitawasaidia katika mahitaji na utatuzi wa changamoto za kifedha pindi zinapojitokeza.

Aidha ameitaka benki ya NMB kuendelea kuandaa program mbalimbali kwa makundi mbalimbali ya watumishi na wananchi kiujumla ili kuwapatia fursa ya kujua huduma zitolewazo na benki pamoja na kubuni bidhaa na huduma za kawaida ambazo mwananchi wa kawaida ataweza kuzimudu.

Pamoja na hayo amewapongeza sana walimu kwa kuunga mkono juhudi za serikali kwa kufanya kazi kwa ufanisi na kwamba wamekuwa wakifanya kazi kubwa ya kuwaandaa viongozi wa baadae na kwamba serikali itaendelea kuandaa mazingira bora kwa walimu katika kuendelea kutoa huduma bora kwa kuwawekea mazingira rafiki walimu ya kufanyia kazi na kuwa Serikali itaendelea kufanya kazi katika kuboresha maisha ya watanzania kwa vitendo.

Kwa upande wake Meneja Mwandamizi Kitengo cha Wateja Maalum Queen Kinyamagoha amesema benki ya NMB imeendelea kuja na suluhisho mbalimbali kwa makundi mbalimbali ikiwemo walimu kama njia mojawapo ya kuleta watanzania kwenye mifumo  rasmi ya kifedha na kuipatia Serikali mapato kwa kuwafikia watanzania wengi zaidi hivyo kuchangia idadi ya watanzania wanaotumia huduma za kibenki.


Pamoja na hayo kwa niaba ya NMB amesema NMB wataendelea kuja na suluhu bora na nafuu kwa watanzania  na kwamba uwajibikiaji wao kwa jamii utabaki kuwa wa viwango vya juu pamoja na kuendelea kushirikiana na Serikali katika kusukuma mbele maendeleo ya kiuchumi ya Taifa na wananchi kiujumla.

Nao walimu kwa nyakati tofauti wameishukuru benki ya NMB kwa huduma mbalimbali ikiwemo uwepo wa mikopo yenye riba nafuu inayotolewa kwa watumishi wa makundi mbalimbali kwani imekuwa msaada kwao katika kuwasaidia kujikimu kimaisha na kuwawezesha kufanya shughuli mbalimbali huku wakishukuru kwa elimu inayoendelea kutolewa na benki hiyo ambayo inawasaidia kupata uelewa zaidi juu ya huduma mbalimbali za kifedha.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa