• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WALIOPOTOSHA MIPAKA YA KIJIJI CHA MABWEGERE WACHUKULIWE HATUA - WAZIRI ARDHI

Posted on: October 1st, 2018

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi ametoa agizo kwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo kuwachukulia hatua  Mkurugenzi Msaidizi wa Upimaji na Ramani wa wizara hiyo pamoja na maafisa wote waliohusika katika upotoshaji wa mipaka ya eneo la Mabwegere  ambayo kwa namna moja ama nyingine umeigharimu Serikali fedha nyingi ili kutatua mgogoro huo.

Agizo hilo limetolewa na Waziri huyo wakati akikabidhi  taarifa ya uchunguzi  iliyofanywa na Jaji wa Mahakama Kuu ambaye kwa sasa ni Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacob Mwambegele kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt Kebwe Stephen  Kebwe  kuhusiana na mgogoro wa mipaka ya kijiji cha Mabwegere na vijiji jirani vya Matongolo, Dumila, Mbigiri, Mfulu na Mambwegwa vilivyopo wilayani Kilosa.

Lukuvi amesema kuwa taarifa ya uchunguzi ilibaini  chanzo cha mgogoro  huo ni kukosekana kwa ushirikishwaji wa vijiji jirani katika kuainisha  na kuweka mipaka  ya kijiji cha Mabwegere jambo lililosababisha  kijiji hicho kuwa na eneo la ukubwa wa hekta 10,234 huku kijiji mama cha Mfulu  kikiwa na hekta 1,717 jambo linalodhihirisha  kwamba mipaka ya kijiji cha Mabwegere kuingia katika  kata tatu za Mbigiri, Kitete na Msowero japokuwa kiutawala kijiji cha Mabwegere  kinaratibiwa na kata ya Kitete

Aidha niseme wazi  Wizara ya Ardhi haijakifuta kijiji cha Mabwegere  bali itaanza kutekeleza  mapendekezo yaliyotokana na uchunguzi ya kufuta mipaka  ya kijiji hicho ambapo kwa sasa utaanza mchakato wa kuanzaa upya mipaka  ya vijiji hivyo kwa njia shirikishi chini ya TAMISEMI kwa kushirikiana na Wilaya ya Kilosa.

Kwa mujibu wa taarifa ya jaji Jacob alipendekeza uboreshwaji wa utendaji kazi, weledi, maadili, umakini na uwezo wa kutunza nyaraka za Idara ya Upimaji  na Ramani kwa ajili ya kumbukumbu jambo litakalosaidia kuepukwa kwa migogoro ambayo inaweza kuzuilika.

Lukuvi  amesema kuwa kuwa Serikali inaelekea kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwakani hivyo ni jukumu la TAMISEMI kwa kushirikiana  na Wilaya ya Kilosa kuhakikisha mipaka inaandaliwa upya kwa ajili ya kuanzishwa kijiji upya.

Na nisisitize kuwa shughuli za kibinadamu kama vile ufugaji na kilimo hazihusiani na masuala ya mipaka, hivyo wilaya licha ya kushughulikia  suala la mipaka lazima iandae mpango wa matumizi bora ya ardhi na kupendekeza maeneo ya ufugaji huku busara ikitumika  kufanya shughuli hiyo.

Naye Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Joseph Kakunda amesema wataalam wanapaswa kuacha nidhamu ya woga bali wazingatie kanuni, sheria na taratibu ili kutekeleza majukumu yao na amemwagiza Katibu Mkuu TAMISEMI kuunda timu ya uchunguzi kuchunguza mchakato mzima wa uanzishwaji wa kijiji hicho na kila atakayebainika  hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi yake.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Kilimo Mary Mwanjelwa amesisitiza hatua za kisheria kuchukuliwa kwa wote waliohusika  na kusema kuwa Serikali ya awamu ya tano inawajali wananchi wake na iko tayari kutetea maslahi ya wananchi, hivyo haitasita kufukua makaburi lengo ikiwa ni kubaini wote walioidanganya serikali.

           

Tangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA WAHE. MADIWANI May 22, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • WAUGUZI WATAKIWA KUWA WAADILIFU MAHALI PA KAZI

    May 30, 2025
  • WAHE. MADIWANI WAISHUKURU SERIKALI YA AWAMU YA SITA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    May 30, 2025
  • KILOSA YAJIPANGA KUTATUA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

    May 28, 2025
  • VITENGO VYA HABARI SERIKALINI VIIMARISHWE KWA KUFANYA MAWASILIANO YA KIMKAKATI

    May 24, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa