• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WANANCHI WA KATA YA MTUMBATU WANUFAIKA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

Posted on: September 17th, 2025

Wananchi wa Kata ya Mtumbatu Wilayani Kilosa wamenufaika na huduma mbalimbali zinazotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Kupitia Divisheni ya Maendeleo ya Jamii ikiwemo kliniki ya utoaji wa mikopo ya Asilimia 10 kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Mikopo ya Wafanyabiashara Ndogondogo Fedha kutoka Serikali kuu ( WBN) kupitia Benki ya NMB, huduma ya bima ya afya iliyoboreshwa (ICHF), Usajili wa NGOs, Vikundi na Huduma ndogo za Kifedha, Kufungua Akaunti, huduma za kisheria na Maswala ya Ukatili na Unyanyasaji wa Kijinsia.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa zoezi hilo, Mratibu wa Mikopo ya 10% wa Halmashauri  ya Wilaya ya Kilosa Ndg William J. Mlay amesema kliniki hiyo imeanza rasmi Agosti 17, 2025 na itafanyika katika Tarafa zote Saba Wilayani Kilosa.

"Tumeanza na Tarafa ya Magole katika Kata ya Mtumbatu ambapo tutakuwepo  kwa siku mbili na lengo kuu ni kusogeza huduma kwa jamii ili kuwafikia wananchi katika maeneo yao". Alisema Mlay

Mlay ameongeza  kuwa wanufanika wa huduma hizo ni wananchi wote wa kata hiyo.


Naye Afisa Dawati la Msaada wa Kisheria Kilosa Ndg. Mladiga Lubele amesema wanatoa ushauri wa Kisheria kwa Wananchi wenye changamoto za kisheria ikiwemo  masuala la ardhi, mirathi na kutoa usuluhishi wa migogoro kwa njia mbadala.

 Kwa upande wake Afisa Mwandikishaji wa bima iliyoboreshwa CHF, Ndg. Abiney Mhina amewashauri wananchi kujiunga na bima hiyo kwani itawasaidia kupunguza gharama za 

hospital ambapo bima hiyo inatolewa kwa watu wasiozidi 6 kwa kaya moja kwa gharama ya Tshs. 30,000/= kwa Mwaka mzima.

Aidha, Bi.Pendo Patrick mkazi wa Kitange kata ya Mtumbatu amesema amepokea vizuri huduma hizo kwani imewarahisishia kupata huduma zote kwa karibu bila gharama yoyote.



Tangazo

  • TANGAZO LA MAFUNZO YA UDEREVA WA MAGARI, PIKIPIKI NA BAJAJI September 30, 2025
  • TANGAZO LA TOZO September 10, 2025
  • TANGAZO LA KUKODISHA MASHAMBA YA HALMASHAURI September 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA WA DARASA LA SABA November 23, 2023
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • WANANCHI WILAYANI KILOSA WAHIMIZWA KUFANYA UCHUNGUZI WA AWALI WA SARATANI YA MATITI

    October 01, 2025
  • WASIMAMIZI WA MIRADI NGAZI YA SHULE WATAKIWA KUFANYA TATHMINI KWA KILA HATUA YA UJENZI

    September 28, 2025
  • KILOSA YAFANIKIWA KUCHANJA MBWA WENGI KATIKA WIKI YA KICHAA CHA MBWA

    September 28, 2025
  • WANANCHI WA KIJIJI CHA MAGUHA KUNUFAIKA NA MASHINE YA KUCHUJA ASALI

    September 21, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa