• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WANANCHI WAASWA KUACHA KUTUMIA MIGOGORO KUJIKIMU KIMAISHA - LUGOLA

Posted on: March 16th, 2019

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh Kangi Lugola ametoa onyo kwa wananchi kuacha tabia ya kutumia migogoro kama njia ya kuendesha maisha na kujipatia kipato kutokana na fedha ambazo wamekuwa wakiwachangisha wananchi kwa kisingizio cha kuwa wasemaji katika kuwasilisha kero za wananchi kwa viongozi wakubwa.

Kangi amesema hayo Machi 15 mwaka huu katika mkutano wa hadhara alipotembelea wilaya ya Kilosa katika kata ya Kimamba na kusema kwamba wapo baadhi ya watu ambao wamekuwa wakitumia migogoro hiyo kama njia ya kujinufaisha na kujikimu kimaisha kwa kushawishi wananchi wanyonge kukusanya fedha ikiwa ni gharama za kuwawezesha kusafiri hali wakijua fedha hizo hazitumiki kama ilivyokusudiwa.

Sambamba na hayo amewataka wananchi wote kwa ujumla kuachana na hulka ya malumbano na badala yake inapotokea migogoro watumie njia stahiki ikiwemo mabaraza ya ardhi kutatua kero zao kwani vyombo hivyo vipo kwa ajili yao na kwamba kwa kufanya hivyo kutaepusha migogoro isiyo na tija lakini pia amewataka wananchi wenye nguvu ya kifedha kutambua kuwa si ruksa kwa mwananchi yoyote kutumia nguvu ya kifedha ili kupora haki za watu.

Aidha amelitaka jeshi la polisi kufanya kazi zao kwa weledi ikiwemo kulinda raia na mali zao ikiwemo ardhi badala ya kuwatishia na kuwakamata wananchi wanapodai haki zao, huku akiwataka polisi hao kuhakikisha amani inatawala na kwamba askari yoyote haruhusiwi kushiriki katika kupora haki za watu na kwamba wapo kutekeleza amri zilizoamriwa na mahakama  ili kuhakikisha mwananchi anapata haki yake.

Kwa upande wa migogoro ya ardhi inayoendelea husuani  mgogoro wa ardhi wa shamba la Mauzi Estate Kangi amewataka wananchi kutambua kuwa suala hilo litasimamiwa na Kamishina wa Ardhi na kwamba kwa sasa liko katika sehemu husika linashughulikiwa hivyo wananchi hao wawe watulivu mpaka hapo maamuzi yatakapotolewa.

Pamoja na hayo Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi amewataka wananchi kuacha tabia ya kuibua migogoro ambayo ipo katika hatua za utatuzi au iliyotatuliwa pindi wanapotembelewa na viongozi hususan mawaziri kwani viongozi wa Wilaya w hiyoapo ili kutatua migogoro, wakati huo huo Mwenyekiti wa CCM Wilaya Ameir Mbarak amewataka wananchi kuwa wakweli na kuacha tabia ya kauli za uchochezi baina ya viongozi na viongozi na kwa upande wa chama wako vizuri na wako tayari kushughulikia kero za wananchi kupitia madiwani wao.

  

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa